Na Beatrice Lyimo- Maelezo.
Kampuni ya COMPULYNX Tanzania inayoshughulika na usambazaji wa
mashine za Electronic Fiscal Device (EFD) imewashauri wafanya biashara nchini
kutumia mashine hizo ipasavyo kwani husaidia kukuza pato la Taifa.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Bw Sailesh Savani
wakati akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
“Wafanyabiashara wasiwe waoga kutumia mashine za EFD kwani huleta uhalali
wa pande zote mbili ikiwemo Serikali na wafanyabiashara hivyo kupelekea
maendeleo ya nchi kwani kodi zitakusanywa kihalali” aliongeza Bw Savani.
Ameongeza kuwa mashine hizo husaidia kuweka kumbukumbu wa mfumo mzima
wa biashara hivyo kuwasaidia wafanyabiashara kujua mapato na ulipaji wa kodi
unaofanyika kihalali na kupelekea Serikali kujua mapato yapatikanayo nchini.
“Ukwepaji wa kulipa kodi umechangia maendeleo duni katika sekta ya Miundo
mbinu pamoja na ukosefu wa huduma za jamii zikiwemo Maji, Hospitali na Elimu
bora nchini”, alifafanua Mkurugenzi huyo.
Mbali na hayo kampuni hiyo inafanya shughuli mbalimbali zikiwemo kusambaza
mitambo ya kieletroniki inayosaidia kukamata wahalifu katika maeneo mbali mbali
ya biashara ikiwepo benki na maduka makubwa.
Pia kampuni hiyo ilifanya mashindano ya uimbaji iliyowashirikisha nchi tatu
ikiwemo Tanzania, Kenya na Uganda na kumtangaza Bw. Tulizo Kaduma kutoka
Tanzania kuwa mshindi wa shindano hilo.
Mkurugenzi Mkuu na Muasisi wa Kampuni ya Compulynx Tanzania
Bw.Sailesh Savani akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es
Salaam alipokuwa akikabidhi Hundi kwa mtunzi wa wimbo wa kampuni
hiyo Kanda ya Afrika Mashariki.
Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Kampuni ya
Cumpulynx Tanzania) Bw. James Alvan (wa kwanza kushoto) akifafanua
jambo kuhusu mashine za Eletronic Fiscal Device(EFD) zinazosambazwa
na Kampuni hiyo kwa Tanzania.
Mkurugenzi Mkuu na Muasisi wa Kampuni ya Compulynx Tanzania
Bw.Sailesh Savani (kushoto) akikabidhi hundi kwa mshindi wa shindano la
ubunifu kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo kwa Afrika Mashariki
Bw.Tulizo Kaduma (Kulia) na katikati ni Afisa Biashara wa Kampuni hiyo
Bi.Genesis Mwaipopo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...