Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe akisisitiza jambo kwa wadau mbalimbali wa habari toka nchi za ukanda wa Afrika Mashariki mapema hii leo wakati akifunga kongamano la siku mbili la wadau wa habari liloandaliwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki lenye lengo la kuangalia mchango wa vyombo vya habari katika kukuza demokrasia katika nchi za ukanda wa Afrika Mashariki.
Mhariri wa gazeti la Hoja toka nchini Tanzania Bw. Yassin Sadik akichangia mada wakati wa kufunga kongamano la siku mbili la wadau wa habari liloandaliwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki lenye lengo la kuangalia mchango wa vyombo vya habari katika kukuza demokrasia katika nchi za ukanda wa Afrika Mashariki mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Bw. Kajubi Mukajanga akimkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe kufunga kongamano la siku lilowashirikisha wadau mbalimbali wa habari toka nchi za ukanda wa Afrika Mashariki mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau wa habari toka nchi mbalimbali za ukanda wa Afrika Mashariki wakiimba kwa pamoja wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakati wa kufunga kongamano la siku mbili la wadau wa habari liloandaliwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki lenye lengo la kuangalia mchango wa vyombo vya habari katika kukuza demokrasia katika nchi za ukanda wa Afrika Mashariki mapema hii leo jijini Dar es Salaam. Picha zote na Eliphace Marwa - MAELEZO
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...