MUFTI Mkuu wa Tanzania,
Sheikh Issa Bin Shaaban Simba,
enzi za uhai wake.
Sheikh Issa Bin Shaaban Simba,
enzi za uhai wake.
Habari zilizofika chumba chetu cha habari mapema asubuhi leo na kuthibitishwa na mamlaka husika zinasema Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Issa Bin Shaaban Simba, amefariki dunia alfajiri ya leo katika hospitali ya TMJ jijini Dar es Salaam.
Habari hizo zinasema mwili wa marehemu umeondolewa hospitali hapo na kuhamishiwa hospitali kuu ya Jeshi ya Lugalo kungoja taratibu za mazishi.
Kwamujibu Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum
amesema kuwa marehemu alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo pamoja na presha.
Mwili wa marehemu utasafirishwa kesho mkoani Shinyanga kwaajili ya maziko.
Tutaendelea kuwaletea taarifa zaidi
kwa kadri zitapopatikana.
Habari hizo zinasema mwili wa marehemu umeondolewa hospitali hapo na kuhamishiwa hospitali kuu ya Jeshi ya Lugalo kungoja taratibu za mazishi.
Kwamujibu Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum
amesema kuwa marehemu alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo pamoja na presha.
Mwili wa marehemu utasafirishwa kesho mkoani Shinyanga kwaajili ya maziko.
Tutaendelea kuwaletea taarifa zaidi
kwa kadri zitapopatikana.
Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un
إِنَّا للهِ وَإِنَّـا إِلَيْهِ رَاجِعونَ)
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara (Mb.) ametuma salamu za rambirambi kwa Baraza Kuu la Waislamu Nchini (BAKWATA) na Waislamu wote nchini kufuatia kifo cha Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti Shaaban Issa Bin Simba kilichotokea Jumatatu, tarehe Juni 15,2015 katika hospitali ya TMJ Jijini Dar es Salaam alipokuwa anatibiwa.
Katika salamu hizo, Mhe. Mukangara amesema kuwa ni jambo la kusikitisha kumpoteza kiongozi huyo ambaye bado Taifa lilikuwa likimuhitaji hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu wa mwezi Oktoba mwaka huu.
Waziri huyo ameongeza kuwa Mufti atakumbukwa kwa upole , unyenyekevu wake na kutopenda makuu,wakati wa uhai wake marehemu alikuwa tayari kumsikiliza kila mtu bila kujali dini au kabila lake.
“Nimepokea kwa huzuni nyingi taarifa ya kifo cha Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti Shaaban Issa Bin Simba ambaye alikuwa Kiongozi anayeshirikiana vizuri na viongozi wote wa serikali na vyama mbalimbali katika kuhakikisha Watanzania wanaendelea kuwa wamoja” amesema .
Amesema Waziri Mukangara: “Nakutumia salamu zangu za rambirambi wewe Katibu Mkuu, BAKWATA na waislamu wote nchini na naungana nanyi katika kuomboleza msiba huu mkubwa katika nchi yetu.
Aidha, kupitia BAKWATA, natuma salamu za dhati ya moyo wangu kwa familia ya marehemu kwa kumpoteza mpendwa wao. Napenda wajue kuwa msiba wao ni msiba wangu. Pia, naungana nao katika kumwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema aiweke pema peponi roho ya marehemu … Amina.”
Imetolewa na;
Idara ya Habari(MAELEZO)
15 Juni,2015
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara (Mb.) ametuma salamu za rambirambi kwa Baraza Kuu la Waislamu Nchini (BAKWATA) na Waislamu wote nchini kufuatia kifo cha Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti Shaaban Issa Bin Simba kilichotokea Jumatatu, tarehe Juni 15,2015 katika hospitali ya TMJ Jijini Dar es Salaam alipokuwa anatibiwa.
Katika salamu hizo, Mhe. Mukangara amesema kuwa ni jambo la kusikitisha kumpoteza kiongozi huyo ambaye bado Taifa lilikuwa likimuhitaji hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu wa mwezi Oktoba mwaka huu.
Waziri huyo ameongeza kuwa Mufti atakumbukwa kwa upole , unyenyekevu wake na kutopenda makuu,wakati wa uhai wake marehemu alikuwa tayari kumsikiliza kila mtu bila kujali dini au kabila lake.
“Nimepokea kwa huzuni nyingi taarifa ya kifo cha Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti Shaaban Issa Bin Simba ambaye alikuwa Kiongozi anayeshirikiana vizuri na viongozi wote wa serikali na vyama mbalimbali katika kuhakikisha Watanzania wanaendelea kuwa wamoja” amesema .
Amesema Waziri Mukangara: “Nakutumia salamu zangu za rambirambi wewe Katibu Mkuu, BAKWATA na waislamu wote nchini na naungana nanyi katika kuomboleza msiba huu mkubwa katika nchi yetu.
Aidha, kupitia BAKWATA, natuma salamu za dhati ya moyo wangu kwa familia ya marehemu kwa kumpoteza mpendwa wao. Napenda wajue kuwa msiba wao ni msiba wangu. Pia, naungana nao katika kumwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema aiweke pema peponi roho ya marehemu … Amina.”
Imetolewa na;
Idara ya Habari(MAELEZO)
15 Juni,2015
Innalilah wainailah Rajiun.
ReplyDeleteInna lillahi, waina ilayhi raajiuun. Pole kwa Familiya ya Sheikh wetu, na pole kwetu sote waislam. Allahumma ghfirlahuu, warhamahuu, waskanahuu filjannah! Aamin.
ReplyDeleteInnalillaahi wa inna ilayhi raajiun....
ReplyDeleteYaarab mfanyie nyepesi hesabu yake.
ReplyDeleteYaarab mpe kauli thabit, yaarab lijaalie kaburi lake liwe bustani katika bustani za Peponi.
AMEEN.
Innaa liLlaahi wa innaa ilayHi raajiuwn.
ReplyDeleteMay Allaah waive any sins and multiply his reward. Amiyn.
Inna lillahi wa inna ilayhi rajeoun!
ReplyDeleteInna lillahi wa inna ilayhi raji'un
ReplyDeleteNimeshtushwa na kusikitishwa na taarifa ya kuondoka kwa Mufti Simba. Natoa pole kwa ndugu na marafiki wa marehemu, na wa-Islam. Ni pigo kubwa kwa Taifa. Mimi kama mwalimu nilikuwa ninamwenzi Mufti Simba kama kiongozi aliyekuwa anahamasisha elimu. Niliwahi kuandika hivyo.
ReplyDeleteMungu amweke mahala pema Peponi.