CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO
(CHADEMA)
SALAAM ZA POLE NA RAMBIRAMBI MSIBA WA MUFTI MKUU SHEIKH SIMBA
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepokea kwa masikitiko na majonzi makubwa taarifa za msiba wa Mufti Mkuu wa Tanzania Tanzania, Sheikh Issa Shaaban bin Simba, Kiongozi Mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kilichotokea asubuhi ya leo kwa maradhi ya sukari na shinikizo la moyo.

Akitoa salaam za pole na rambirambi kwa waumini wa madhehebu ya Kiislamu na Watanzania wote kwa ujumla baada ya kupata taarifa za msiba huo, Mwenyekiti wa CHADEMA (T), Freeman Mbowe amesema kuwa Mufti Mkuu Simba atakumbukwa kwa namna aliyosimama kama kiongozi wa dini kupitia kauli zake mara kwa mara akisisitiza ushirikiano ndani ya jamii ya Watanzania bila kujali tofauti zao katika itikadi za dini.

“Mara kwa mara Mufti Mkuu Simba amesikika akiwaambia Watanzania, si Waislam pekee aliokuwa akiwaongoza kiroho, hata wale wanaoamini katika madhehebu tofauti, umuhimu wa kudumisha ushirikiano miongoni mwa dini mbalimbali na makundi mengine katika jamii ikiwa ni mojawapo ya misingi ya kuimarisha umoja wa taifa letu.”

“Naungana na Waislam wote nchini katika wakati huu wa kuomboleza kifo cha kiongozi huyu wa kiroho. Kwa niaba ya niaba ya uongozi wa CHADEMA, wanachama, wapenzi na wafuasi, natoa salaam za pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki, BAKWATA, viongozi wa kiroho nchini na Watanzania wote ndani na nje ya nchi walioguswa na msiba huu mzito.”

“Mwenyezi Mungu awatie nguvu wote na kuwafanyia wepesi katika wakati huu mgumu wa majonzi ya msiba wa Mufti Mkuu Simba,” amesema Mbowe
Inna Lillahi wa inna ilaihi raji’un.

Imetolewa leo Jumatatu, Juni 15, 2015 na;
Idara ya Habari na Mawasiliano- CHADEMA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...