· Wasanii kutoka Afrika, Mashariki ya Kati na Asia kunufaika na huduma hii.
Abu Dhabi – Kampuni ya Clouds Media International leo imetangaza kuzindua huduma mpya ya kutafuta na kuwaunganisha wasanii kwenye nafasi za kutoa burudani kwenye matamasha na matukio mbalimbali.
Kazi hiyo ya kuunganisha na kuwatafutia wasanii nafasi ya kutoa burudani itakuwa chini ya Status Bookings ambayo ni kampuni dada ya Clouds Media Group.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Clouds Media, Joseph Kusaga, uzinduzi wa huduma hii ni muendelezo wa kawaida wa kukua kwa kampuni yake.

Tamasha la Fiesta linaloandaliwa na Primetime Promotions ni moja ya tamasha kubwa zaidi Afrika na sasa linaingia mwaka wa 15 likiwa na wahudhuriaji zaidi ya 400,000 kwa mwaka.
Huduma hii ya kutafuta na kuwaunganisha wasanii itakuwa inasimamiwa kutoka makao makuu ya Status Communications yaliyoko Abu Dhabi huku yakipata ushirikiano kutoka ofisi za Status zilizoko Dar es Salaam, Tanzania pamoja na Nairobi, Kenya.
Huduma hii itawapa nafasi waandaji wa shughuli za burudani pamoja na makampuni mbalimbali kuwasiliana na kupata wasanii mbalimbali kutoka chanzo kinachoaminika.
Afsa Mwendeshaji Mkuu wa kampuni ya Status anasema huu ni wakati muafaka wa kuingia kwenye huduma ya kuunganisha na kuwatafuta wasanii nafasi ya kuburudisha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...