Wafanya biashara wadogo huamini kwamba kua na tovuti ni kitu kinachofanywa na wafanya biashara wakubwa na inaitaja gharama nyingi kutengeneza. Hilo sio kweli. Gharama ya kuwa na website ni ndogo sana ukilinganisha na faida utakazo zipata baada ya kuwa nayo. Faida ya kuwa na tovuti ni pamoja na; Biashara yako kuaminika kitaifa na kimataifa. Biashara zote zilizo halisi na zinazoaminika hua na tovuti. Tovuti yako itasaidia kuhalalisha biashara yako. Kuwa na tovuti pia itakusaidia kujitangaza kwa bei rahisi sana kuliko utangazaji wa magazeti, radio, mabango na mwingine wowote.  Kwa kuwa tovuti ipo mtandaoni masaa 24 na mahali popote hivyo basi wateja wako wataweza kukuona mahali popote watakapo kuwa na kwa muda wowote. 

Pamoja na hayo mabadiliko yoyote yatakayo tokea kwenye biashara yako yanaweza kusambazwa kiurahisi kwa wateja wako. Ukiongeza bidhaa unazo uza, ukiongeza au ukibadalisha huduma unazozitoa nk. wateja wako wanapata huu ujumbe kiurahisi bila gharama zozote kwako.  

Kutengenezea tovuti ya biashara yako, tumia wasajili wa tzNIC wenye vibali vinavyokubalika: http://www.tznic.or.tz/index.php/registrars/accredited-registrars.

Au, unaweza kwenda moja kwa moja kwenye tovuti ya tzNIC. Kama una maswali zaidi tembelea kurasa zao za Facebook na Twitter

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...