Na Bashir YAkub
Sura  ya  29  Sheria  ya ndoa  imeeleza  mambo  mengi . Baadhi  yanajulikana  na  baadhi  hayajulikani.  Wakati  mwingine  hata  baadhi  ya yanayojulikana   haijulikani  kama  yameruhusiwa  na  sheria  au  yanafanyika  kimazoea.  Na  hapa  ndipo  inapoibukia  migogoro mingi  ambayo  tunayoshuhudia  mahakamani  na  hata nje  ya  mahakama. Aidha  sheria  hii  imebeba  mambo  mengi  ya  talaka, matunzo  ya  watoto  na  mwanamke, jinai  za  unyanyasaji  wa  kijinsia, ndoa  haramu  na  halali  na mengine  mengi  kuhusu  familia  na  ndoa. Mengi  kati  ya haya  yameishaelezwa  kwa  anayetaka  kuyajua  basi   atembelee SHERIA  YAKUB  BLOG  atafute atapata  humo.

 Leo  ni  muhimu  kuzungumzia  jambo  jingine  muhimu   ambalo  nalo  limekuwa  likitatiza   na kuleta  shida  kwa  wanandoa. Ni  kuhusu   ruhusa  ya kuoa  na  kuoa  mke  zaidi  ya  mmoja. Ndoa  zipo  aina  nyingi  na  upo  uhuru  wa  mtu kufunga  ndoa  kutokana  na  maamuzi   yake  na  mwenza  wake  wanavyoamua.  
Yumkini   unapoamua  kufunga  ndoa  ya  aina  fulani  yakupasa  pia  uwe  umejua  matokeo, athari  za  ndoa  hiyo. Kila  aina  ya ndoa utakayofunga   ujue  wazi  kuwa  itaambatana  na   haki  fulani  , wajibu  fulani  na  mipaka  fulani.  Hakuna  ndoa utakayoifunga  iwe moja  kwa  moja bila  mipaka  .  Na  hili  hasa  ndilo  linalojadiliwa  na  makala  haya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...