Mke wa Rais
Mama Salma Kikwete akielekea kwenye ukumbi wa mkutano wa Sandton Internationa
Center unakofanyika mkutano wa wake wa Marais na Wakuu wa Nchi za Afrika huko
Johannesburg nchini Afrika Kusini tarehe 15.6.2015. Aliyefuatana na Mama Salma
ni Mwenyekiti wa OAFLA anayemaliza muda wake Mama Hinda Derby Itno.
Mke wa
Rais Mama Salma Kikwete akiangalia moja ya machapisho mbalimbali yanayohusiana
na Mkutano wa Wake wa Marais na Wakuu wa Nchi za Afrika (OAFLA) unaofanyika
nchini Afrika Kusini.
Wake wa
Marais na Wakuu wa Nchi za Afrika wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya
ufunguzi wa mkutano wao wa mwaka unaozungumzia uwezeshaji kwa wanawake na Maendeleo
katika Bara hili.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa hotuba yake ya mwisho kwenye kikao
cha Wake wa Marais na Wakuu wa Nchi za Afrika kinachofanyika kwenye Ukumbi wa
Sandton jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini tarehe 15.6.2015.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...