Mke wa Thobias Mwanakatwe, Levina Michael Genda, 
enzi za uhai wake.
Mwanahabari Thobias Mwanakatwe, \
akiwa na mke wake enzi za uhai wake.

Dotto Mwaibale

MWANAHABARI wa Kampuni ya The Guardian na Nipashe, Thobias Mwanakatwe, amepoteza mke wake baada ya kugongwa na gari eneo la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam jana usiku majira ya saa 2:30.
Akizungumza na mtandao wa www.habari za jamii.com. Mwanakatwe amesema kifo cha ghafla cha mke wake ni pigo kubwa kwake na familia zote mbili.
Mwanakatwe amesema shughuli za kuuaga mwili wa marehemu zitafanyika kesho kuanzia saa tano na baada ya hapo watausafirisha kwenda kijiji cha Endala Karatu mkoani Arusha kwa mazishi yatakayofanyika kesho kutwa.
Kama kuna yeyote atakaye penda kumtolea chochote mwenzetu Mwanakatwe ili kimsaidie kwa msiba huo anaweza kuwasiliana naye kwa namba hizi za simu-0762-183666, 0655-183666 na 0787184666. 
Bwana alitoa na 
bwana ametwaa jina 
lake lihimidiwe
AMINA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...