THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS


Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Bw. Clement Mshana, wafanyakazi wake na waandishi wote kwa ujumla kufuatia kifo cha mtangazaji na mwandishi mwandamizi wa TBC Bi. Florence Dyauli.
“Pokea rambirambi zangu za dhati kwa kuondokewa na mwandishi mwandamizi na mahiri Bi. Florence” Rais amesema
“Mbali na uandishi na utangazaji wake mahiri, Bi. Florence alikua mzalendo wa kweli aliyetumikia taasisi hii ya serikali kwa uadilifu na upendo wa kweli, tutamkumbuka na tutaukosa mchango wake. Ni wajibu wetu kumuombea mapumziko mema kwa mwenyezi Mungu na kumshukuru kwa mchango wake alioutoa kwa moyo wa dhati”. Amesema Rais Kikwete na kuongeza kuwa:
“Hakika Florence tutamkumbuka, nawapa pole wafanyakazi wote wa TBC na waandishi wote kwa kuondokewa na mwenzao katika tasnia ya Habari”. Rais ameongeza.
“Salaam pia ziwafikie ndugu na jamaa wa Bi. Florence ambao msiba huu ni mkubwa sana kwao na unawagusa sana, naelewa machungu waliyonayo na huzuni, hata hivyo kwa pamoja ni wakati wa kuzidi kumuombea Marehemu katika safari yake ya mwisho”. Rais amesema na kuwatakia roho ya subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu kwao.
Bi. Florence ambaye amefariki jana  18 Juni, 2015 jijini Dar-es-Salaam alizaliwa Julai 27, 1961. Bi. Florence alianza kazi katika Radio ya Taifa, Radio Tanzania Dar-es-Salaam (RTD) na baadaye  Televisheni ya Taifa (TVT) na kwa sasa TBC .
Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahali pema peponi, Amina.
Imetolewa na:
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi,
Ikulu-DSM
19 Juni, 2015

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...