THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1 BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amepokea kwa mshutuko na masikitiko taarifa za kifo cha mbunge wa Jimbo la Ukonga, Dar es Salaam, Mheshimiwa Eugenia Mwaiposya ambaye ameaga dunia usiku wa kuamkia jana, Jumanne, Juni 2, 2015, mjini Dodoma ambako alikuwa anahudhuria Vikao vya Bunge.

Katika salamu zake za rambirambi kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Anna Makinda, Rais Kikwete amesema: “Nimepokea kwa mshutuko na masikitiko taarifa za kifo cha Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Eugenia Mwaiposya ambaye nimejulishwa ameaga dunia mjini Dodoma ambako alikuwa anaendelea kuhudhuria Vikao vya Bunge.”

Amesema Rais Kikwete: “Kwa hakika, taifa letu limepoteza kiongozi muhimu kutokana na kifo hiki. Mbunge Mwaiposya alikuwa mwakilishi hodari na mtetezi wa kuaminika wa wananchi wa Jimbo la Ukonga. Napenda kukutumia wewe Mheshimiwa Spika salamu zangu za rambirambi kwa kupoteza Mbunge mahiri sana. Aidha, kupitia kwako, nawatumia Wabunge wote salamu zangu za rambirambi kwa kuondokewa na mwenzao.”

Ameongeza Rais Kikwete: “Kupitia kwako, Mheshimiwa Spika, napenda pia kutuma salamu zangu kwa wananchi wa Jimbo la Ukonga ambao wamepoteza mwakilishi wao. Mheshimiwa vile vile, napenda kutoa pole nyingi kwa familia, ndugu na jamaa wa Mbunge Mwaiposya kwa kuondokewa na mama na mchangiaji mkubwa katika maisha yao. Wajulishe niko nao katika msiba huu mkubwa. Naelewa uchungu wao katika kipindi hiki na nawaombea subira ili waweze kuvuka kipindi hiki. Naomboleza nao na naungana nao katika kumwomba Mwenyezi Mungu aiweke peponi roho ya Mheshimiwa Eugenia Mwaiposya. Amina.”

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

2 Juni, 2015




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...