Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa atuma salamu za Rambirambi kwa BAKWATA kufuatia kifo
cha Mufti Issa Bin Shaaban Simba.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin Mkapa, amemtumia Kaimu Mufti wa Tanzania, salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Mufti Issa Bin Shaaban Simba kilichotokea Jumatatu katika hospitali ya TMJ.
Katika salamu zake Mhe. Mkapa ameelezea kushtushwa kwake na kifo cha Mufti Simba ambae amemuelea kama kiongozi “aliyekuwa muadilivu, mpenda amani, mwenye busara na mbobevu mkubwa wa masuala yanayohusu dini ya kiislamu”. Kwenye salaamu zake Mhe, Mkapa amemuelezea Marehemu Mufti Simba kuwa alikuwa “kiungo muhimu sio tu kwa waislamu bali hata kwa serikali na jumuiya za dini mbali mbali”.
Ametoa pole zake kwa BAKWATA, familia ya Marehemu Mufti Simba, waislamu wote na watanzania kwa ujumla kwa msiba huu; na amewaombea kwa mungu “awape subira, imani na busara kwenye kipindi hiki kizito”. Aidha, amewaombea BAKWATA mungu awape “busara na hekima zaidi za kuweza kuendelea kuijenga taasisi hiyo kama ambavyo Marehemu Mufti Simba alifanya ili iendelee kuwa nguzo muhimu ya amani na utulivu nchini mwetu” hasa katika kipindi hiki ambapo nchi inapita katika  mitihani kadhaa.
Inna lillahi wa Inna Ilayhi Rajiuun
Imetolewa na:
Ofisi ya Rais Mstaafu,
Mhe. Benjamin William Mkapa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...