MABALOZI wa Usalama Barabarani nchini Tanzania (Road Safety Ambasadors-RSA) wamekabidhi misaada kwenye Ofisi ya Kitengo cha Mawasiliano cha Kikosi cha Usalama Barabarani cha Jeshi la Polisi nchini (Traffic Control Center-TCC).
Vifaa hivyo ambavyo ni vitendea kazi katika kituo cha taarifa cha Kitengo cha Mawasiliano cha Kikosi cha Usalama Barabarani cha Jeshi la Polisi nchini, vimekabidhiwa jana jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa RSA, John Seka ikiwa ni michango ya mabalozi hao.
Akizungumza katika hafla hiyo ya kukabidhi, Seka alisema lengo la msaada huo ni wa Mabalozi wa Usalama Barabarani ni kutaka kuboresha mawasiliano ya Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani.
Alivitaja vifaa vilivyokabidhiwa kuwa ni pamoja na Radio mbili za mawasiliano za kidijitali, Simu ya mawasiliano aina ya Tablet iliyounganishwa na makundi ya RSA ya Facebook, Whatsapp na Telegram, Mtungi wa Maji ya Kunywa, Viti vya kukalia, Feni na Zulia la Ofisi ya TCC.
Aidha Seka alitaja msaada mwingine ni Birika la kuchemsha maji ya chai, Mfumo wa kutunza betri kwa ajili ya Tablet (Power Bank) na Gharama za Upakaji wa Rangi wa ofisi ya TCC ikiwa vyote vinalenga kuhakikisha ofisi ya TCC inafanya kazi kwa ufanisi na bila vikwazo ili kurahisisha mawasiliano kati ya RSA na TCC.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...