Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akitoa sadaka kwa Watoto Yatima wa kiumewa Kituo cha Kulelea Watoto Yatima cha Rahman kiliopo Chang’ombe Mjini Dodoma hapo kwenye makazi yake Mtaa wa Farahani Mjini Dodoma.Kulia ya Balozi Seif Ali Iddi ni Mkewe Mama Asha Suleiman Iddi.
Balozi Seif Ali Iddi akitoa sadaka kwa Watoto Yatima wa Kike wa Kituo cha Kulelea Watoto Yatima cha Rahman kiliopo Chang’ombe Mjini Dodoma baada ya kufutari nao pamoja.
Baadhi ya Watoto Yatima wa Kituo cha Kulelea Watoto Yatima cha Rahman kiliopo Chang’ombe Mjini Dodoma wakipata futari ya pamoja iliyoandaliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif katika Makaazi yake yaliyopo Mtaa wa Farahani Mjini Dodoma. Picha na – OMR – ZNZ.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesisitiza umuhimu wa Waumini wa Dini ya Kiislamu kuendelea kujenga utamaduni wa kufutari pamoja ili kudumisha utaratibu uliotiliwa nguvu na Kiongozi wa Dini hiyo Mtume Muhammad { SAW } na kuendelezwa na maswahaba waliomfuata.

Balozi Seif ametoa sisitizo hilo kwenye hafla ya Futari ya pamoja aliyowaandalia Watoto Yatima wanaolelewa katika Kituo cha malezi ya Watoto yatima cha Kiislamu cha Rahman Kiliopo Chang’ombe Mjini Dodoma. Futari hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na baadhi ya viongozi wa Dini ya Kiislamu wa Mji wa Dodoma wakiambatana na baadhi ya Viongozi wa Serikali na Kisiasa ilifanyika katika Makazi yake yaliyopo Mtaa wa Farahani Mjini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...