Na SMEs Litakalofanyika Dar Es Salaam BOFYA HAPA
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kwa kushirikiana na Kituo cha Uwekezaji cha Kimataifa (International
Trade Centre UN-Agency) inafanya Maandalizi ya Kongamano la Diaspora (Tanzania Diaspora & SMEs Partnership Conference
2015).
Kongamano husika litafanyika hapa Dar es Salaam, kuanzia tarehe 13 hadi 15
Agosti 2015 katika Hoteli ya Serena. Kongamano hilo litakuwa la pili kufanyika
hapa nchini na litahusisha Diaspora na Wadau wa hapa Tanzania.
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano
wa Kimataifa, Ofisi ya Rais na Utawala Bora – Zanzibar na Ofisi ya Waziri Mkuu
ndio Wadau Wakuu katika Maandalizi ya Kongamano hili.
Kongamano la
mwaka huu lina Kauli Mbiu, ‘Creating Linkages between Diaspora and Local
SMEs in Tanzania’ na Dhumuni lake ni kuhamasisha Ushiriki wa Diaspora
katika kukuza Biashara Ndogo na za Kati hapa nchini. Kongamano la mwaka huu pia
litahusisha Mikoa ya Tanzania ambapo Mikoa itapata fursa ya kutangaza fursa za
uwekezaji zilizopo Mikoani.
Kongamano hilo linatarajiwa
kufunguliwa na Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na kufungwa na Mhe. Dr. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.
Aidha,
katika kuhitimisha kilele cha Kongamano hilo, Diaspora wanatarajiwa kufanya
ziara Zanzibar tarehe 15 Agosti 2015, ikiwa ni sehemu ya mwaliko maalum kutoka
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Pamoja na Shughuli za Ufunguzi na
Kilele, Matukio muhimu yatakuwa ni Maonesho ya Kibiashara, Majadiliano ya Mada kuhusu
Ushirikishwaji wa Diaspora kwa Maendeleo ya Nchi hususan SMEs, uwekezaji
Mikoani n.k.
Kongamano hilo
litahudhuriwa na Watanzania Wanaoishi Ughaibuni (Diaspora) na wale waliorejea
hapa nchini na Wadau wa Maendeleo kutoka hapa nchini.
Wizara ya
Mambo ya Nje inawakaribisha kushiriki nasi katika Kongamano hilo. Tafadhali
tembeleeni tovuti ya (www.tzdiaspora.org)kupata
taarifa muhimu hususan kuhusu Ada za Ushiriki, fursa za Kufadhili na namna ya
kujisajili.
Imetolewa na: Wizara ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa, Dar es Salaam
21 Julai, 2015
TAFADHALI IBANE HII COMMENT.
ReplyDeleteDear Mr. Michuzi, bare with me for using this ‘comment section’ for now. I just found out that two donations I sent to UJENZI WA MSIKITI KIJIJI CHA KIMBANGULILE MKURANGA PWANI were not picked. http://issamichuzi.blogspot.com/2015/05/maombi-ya-mchango-wa-ujenzi-wa-msikiti.html
P/SE use the following info:
DonationOne –> Receiver: GHALIB NASSOR MONERO; Date of Transaction: May 26, 2015; Tracking Number: 651-874-1958; Amount $20.00
DonationTwo –> Receiver: GHALIB NASSOR MONERO; Date of Transaction: July 15, 2015; Tracking Number: 126-030-7230; Amount $20.00
Use a government issued identification – these donations are available for pick up. If by Friday the donations have been picked up, I will send another $20.00 same day.
Thank you very much.