MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali kesi namba 301 iliyofunguliwa na Kampuni ya kufua Umeme ya IPTL, PAP pamoja na Mkurugenzi wa Kampuni ya PAP Bw Harbinder Singh Sethi dhidi ya Mbunge wa Kigoma Kusini Mhe David Kafulila kwa madai kuwa Kafulila alichafua jina kampuni hizo na muhusika huyo kwamba walichota zaidi ya 300bn kwenye akaunt ya Tegeta escrow kinyume cha sheria na taratibu.

Katika shauri hilo, Kampuni ya IPTL,PAP na Herbinder Singh Sethi walitaka Mahakama imuamulu Mhe Kafulila alipe fidia ya 310bn kwa kuchafua jina la kampuni na mkurugenzi huyo.

Katika kesi hiyo Mhe Kafulila alikuwa akitetewa na taasisi za kisheria za Legal& Human Righ Centre pamoja na kituo cha Human Righ Deffenders.

Akitoa uamuzi huo mbele ya mawakili wa Human Right Defenders na Legal & Human Right Center wakiongozwa na wakili Mtobesya huku mawakili wa IPTL, PAP na Sethi wakiwa hawakufika mahakamani, Jaji Rosemary Teemba alisema Mahakama Kuu imejiridhisha kwamba kampuni ya IPTL, PAP na Mkurugenzi wao Harbinder Sethi hawakuwa na hoja za msingi kuthibitisha madai yao kama msingi wa kufungua kesi mahakama kuu na hivyo kwa kuzingatia hali hiyo Mahakama Kuu kanda ya Dar es salaam inatupilia mbali shauri hilo kuanzia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...