Mtangazaji
wa kipindi cha Fema Tv Show,Rebecca Gyumi akizungumza na Waandishi wa Habari
juu ya uzinduzi rasmi wa kipindi hicho cha Fema Tv Show,itakayo anza rasmi
Julai 13 hadi Septemba mwaka huu,huku mmoja wa watangazaji wa kipindi
hicho,Ummy Omary akisikiliza kwa umakini.
Baadhi ya
Waandishi wa Habari wakisikiliza kwa umakini juu ya uzinduzi wa onyesho hilo la
Fema Tv.
Na Bakari Issa, Globu ya jamii.
FEMINA Hip
kwa kushirikiana na asasi zingine za kiraia inatarajia kuanza rasmi kipindi
chake cha Fema Tv Show Julai 13 Mwaka huu, chenye lengo la kuelimisha
jamii kwa ujumla juu ya kuwapa wasichana sauti, nafasi na fursa ya kushiriki
masuala mbalimbali ikiwa ni haki ya elimu, haki ya kupata rasilimali pamoja na
haki ya kushiriki kwa amani.
Akizungumza
leo jijini Dar es Salaam, Mtangazaji wa kipindi hicho cha Fema Tv, Rebecca Gyumi
amesema katika show hiyo utaona program nyingine zinazohusu masuala ya vijana
hususani kuelekea katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu wa 2015.
amesema kuwa katika
kipindi hicho cha Fema Tv Show kitakacho wafikia
vijana wote na jamii nzima pia kitawajibika katika kuibua masuala ya msingi
yanayohusu wasichana.
Pia, amesema
vipindi hivyo vitarushwa kupitia vituo vya utangazaji vya East Africa televisheni siku ya juma pili saa tatu kamili usiku na na Star
TV kitarushwa siku ya jumatatu saa tatu na nusu usiku.
Aidha, amesema
Agenda ya Nguvu ya binti mwaka huu inaweza kubebwa na kuwekwa katika ilani za vyama
vy asiasa na mipango mingine ya asasi za kiraia inayolenga kuibua masuala ya
wasichana na wanawake katika mchakato wa uchaguzi wa mwaka huu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...