Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo ameagana na mabalozi watatu wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania baada ya kumaliza muda wao wa kazi .
Mabalozi walioagana na Rais leo ikulu jijini Dar es Salaam ni pamoja na Mhe.Debnath Shaw wa India,Balozi Koenraad Adam wa Ubelgiji na balozi Lennarth Hjelmaker wa Sweden.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na balozi wa India anayemaliza muda wake Mhe.Debnath Shaw wakati balozi huyo alipokwenda kumuaga ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na balozi Koenraad Adam wa Ubelgiji ikulu jijini Dar es Salaam leo alipokwenda kumuaga.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Balozi wa Sweden nchini aliyemaliza muda wake Mhe.Lennarth Hjelmaker ikulu jijini Dar es Salaam. Picha na Freddy Maro
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...