1
Mwenyekiti wa Klabu ya Coastal Union,Dr.Ahmed Twaha katikati akifuatilia mkutano wake na kamati ndogo ndogo za klabu hiyo uliofanyika jana,kulia ni Katibu Mkuu wa Coastal Union,Kassim El Siagi,
2 3
Mwenyekiti wa Cpastal Union akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Mipango na Fedha mara baada ya kumalizika kikao hicho.
………………………………………………………………………….

UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union umeitaka kamati ya ulinzi na usalama kuhakikisha inatimiza wajibu wake ipasavyo ikiwemo kuhakikisha vitendo vitakavyoweza kuigharimu timu hiyo wakati wa michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara vinazibitiwa.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa kikao baina ya Kamati ndogo ndogo zilizoundwa,Mwenyekiti wa Klabu ya Coastal Union,Dr.Ahmed Twaha alisema kuwa kumekuwa na vitendo vingi ambavyo vinajitokeza kwenye michuano ya Ligi kuu Tanzania bara na kuigharimu timu yetu na kulazimika kulipa faini ambayo ingeweza kufanya mambo mengine ya maendeleo.

Alisema kutokana na kuwepo kwa tatizo hilo ndio sababu pekee iliyopelekea kuundwa kamati hiyo ili kuweza kukabiliana na vitendo vinayoweza kuisababisha hasara ndani ya klabu hiyo kwani vinakwamisha juhudi za kupiga maendeleo.

   “Ukiangalia msimu uliopita tulipata hasara ya shilingi milioni 3 kwa makosa ya uwanjani na hii inasababishwa na mashabiki kitendo ambacho kinaharibu sura ya mkoa hivyo lazima kamati hii italisimamia suala hilo “Alisema Mwenyekiti huyo.

Aidha Mwenyekiti huyo aliitwisha mzigo mengine kamati ya Nidhamu na Maadili kuhakikisha watu wanaotukana kwenye mitandaa ya kijamii ikiwemo Facebook, Twiter na mengineyo watachukuliwa hatua kali za kisheria ili kukomesha vitendo hivyo.
Hata hivyo alisema kuwa kamati hiyo itakuwa na jukumu kubwa la kuhakikisha ulinzi na usalama unaimarishwa wakati wa timu hiyo itakapokuwa ikicheza mechi zake kwenye michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara.

 “Lakini pia zamani wapo watu walikuwa wakitengeneza vitabu vya tiketi na kufanya mapato kuwa madogo licha ya uwepo wa watu wengi hivyo huu ndio mwisho wao kamati hii pia itasimamia suala hilo kwani hali hii iliifanya klabu kukosa mapato “Alisema Mwenyekiti huyo.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa wameweka mipango mizuri ya kuhakikisha timu hiyo inafungua matawi kwenye mikoa yote timu hiyo itakapokuwa ikienda kushiriki michuano ya Ligi kuu hapa nchini.

IMETOLEWA NA OFISA HABARI WA COASTAL UNION.
OSCAR ASSENGA.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...