Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Said Meck Sadick akizindua kampeni ya kuosha Magari katika viwanja vya Leaders Club kwa ajili ya kuchangia Fedha kwa waandishi wa habari ambao wanamatatizo ya Kiafya ikiwemo Saratani ( MEDIA CAR WASH FOR CANCER).
 Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), BW. Assah Mwambene (kulia) akikabidhi kiasi cha fedha kwa Mmoja wa Waratibu wa MEDIA CAR WASH FOR CANCER Bw. Benjamin Thomson, zilizochangwa na Idara hiyo kupitia chama chao cha Maofisa Habari wa Serikali  ambao walichanga kiasi cha shilingi Milioni 1,680,000=. Katikati ni  Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Paul Makonda.

Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na michezo pia imechangia shilingi 1,350,000/= baada ya kuguswa na  kampeni  hiyo adhimu ya kuwachangia waandishi wa Habari wenye Matatizo mbalimbali yakiwemo ya Saratani.

Kampeni hiyo imefanyika leo katika viwanja vya Leaders  Club  Kinondoni jijini Dar es salaam ambapo viongozi mbalimbali wakiwemo na wadau wa habari walishiriki zoezi la kuosha magari kwa kuchangia kiasi chochote cha fedha, Mgeni rasmi akiwa Mkuu wa Mkoa Dar Es Salaam Mhe. Said Meck  Sadick.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Paul Makonda akishiriki kuosha moja ya Magari yaliyofika kuoshwa katika MEDIA CAR WASH FOR CANCER  kuchangia waandishi wa habari wenye magonjwa mbalimbali ikiwemo Saratani.
 Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe akiosha Gari wakati wa  Shughuli hiyo maalum kwa ajili ya Kuchangia waandishi wenye udhoofu wa afya zao (MEDIA CAR WASH FOR CANCER).
Ankali akiosha Moja ya Magari kwa ajili ya kuchangia waandishi wa habari ambao wana maradhi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Saratani
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO Bw. Assah Mwambene akimshukuru Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Paul Makonda mara baada ya kushiriki zoezi la kuwachangia waandishi wa Habari wenye Matatizo mbalimbali yakiwemo ya Saratani (MEDIA CAR WASH FOR CANCER).
 Picha ya pamoja ya waandishi wa 
Habari pamoja na Baadhi ya Viongozi.

Unaweza Changia pia kupitia M-Pesa 0766 970240
au Tigo Pesa 0653 155 808.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...