Mshindi wa shindano la Airtel Trace Music Star Nalimi Mayunga ameachia

kibao chake kipya cha " Nice Couple" video itakayorushwa kuanzia leo
katika kituo cha DSTV chanel ya Trace Urban 325

MWANZONI mwa mwezi huu, Mshindi huyo wa Airtel Trace Music star alitua
mjini Johannesburg South Afrika akitokea nchini Tanzania  ili kuanza
safari yake kujiendeleza kimuziki na kufikia ndoto zake mara baada ya
kuibuka mshindi wa mashindano makubwa yaliyoshirikisha nchi 13 barani
Afrika  yaliyofanyika tarehe 18 April 2015,

Mayunga alitangazwa mshindi na mwanamuziki wa kimataifa wa miondoko ya R& B wa nchini Marekeni , Akon and kupata zawadi nono ikiwemo deli ya


 kurekodi single ambapo mayunga alishuka nchini South Afrika  na

kuredoki nyimbo yake ya "Nice Couple" katika maeneo ya Orlando East.

Nyimbo hii tayari imeshaanza kupigwa katika vyombo na sehemu
mbalimbali nchini South Afrika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...