Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Rished Bade akiongea na wadau
kutoka Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) wakati wa semina ya kuwajengea
uelewa kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2014
iliyoanza kutumika kuanzia Julai 1, 2015, Leo Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
wa Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) Dkt. Samuel Nyantahe akimshukuru
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Rished Bade kwa uamuzi wa
kuwakutanisha wadau wa sekta ya viwanda na kuwaelimisha kuhusu Sheria Mpya ya
Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2014 ili kuweza kuondoa utata kwenye
baadhi ya maeneo yaliyo katika sheria hiyo, Leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) Leodger Tenga akimueleza Jambo
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Rished Bade wakati wa
semina ya kuwajengea uelewa kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani
ya mwaka 2014 iliyoanza kutumika kuanzia Julai 1, 2015, Leo Jijini Dar es
Salaam.
Afisa
Mwandamizi Toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Beldom Chaula akiwaeleza
jambo baadhi ya wadau kutoka Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) wakati wa
semina ya kuwajengea uelewa kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani
ya mwaka 2014 iliyoanza kutumika kuanzia Julai 1, 2015, Leo Jijini Dar es
Salaam.
PICHA
NA HASSAN SILAYO -MAELEZO
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...