Na Mwandishi Wetu
Wasanii
nchini wameiomba Serikali kumalizia ujenzi wa ukumbi wa Sanaa za
maonesho unaojengwa kwa zaidi ya miaka minane sasa makao makuu ya Baraza
la Sanaa la Taifa (BASATA) eneo la Ilala sharif Shamba jijini Dar es
Salaam.
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti kwenye programu ya Jukwaa la Sanaa ya Baraza hilo
mapema wiki hii, wasanii hao walieleza kwamba kwa sasa kuna ufinyu wa
kumbi za za maonesho hali ambayo imekuwa ikiwafanya wasanii hao kukosa
maeneo ya kufanya sanaa zao hivyo kumalizika kwa ukumbi huo itakuwa ni
ahueni kubwa kwao.
“Ukumbi
huu ni muhimu sana kwetu, wengi tuliutazama kama mwanzo wa ufufuaji wa
Sanaa za majukwaani lakini sasa ni muda mrefu hauoneshi dalili za
kumalizika. Kuna kila sababu ya ukumbi huu kukamilika ili kutusaidia
katika maonesho yetu” alisema Msanii Khalid Kambau.
Kwa
upande wake msanii wa Sanaa za maigizo Christian Kauzeni ambaye pia ni
mwenyekiti wa chama cha wasanii waigizaji mkoani Dar es Salaam alisema
kwamba kutokana na ukumbi huo kutazamwa kama mkombozi wa wasanii kuna
kila sababu ya kuangalia mbinu mbalimbali ili kuhakikisha unakamilika
mapema iwezekanavyo.
Awali
akiwasilisha mada kwenye Jukwaa hilo la Sanaa iliyohusu ‘Ubora wa
Filamu na Changamoto zake’ msanii na mzalishaji filamu maarufu nchini
William Mtitu alisema kwamba tasnia ya filamu chini imepata umaarufu na
kukua ingawa bado changamoto za uharamia, elimu na masoko zimeendelea
kuiathiri.
“Kwa
sasa filamu zinazozalishwa zimekuwa na ubora kuliko huko nyuma. Tatizo
liko kwenye elimu kwa wasanii, uharamia na masoko. Kulikuwa na maduka
zaidi ya sabini na tano yanayouza kazi za wasanii wa filamu lakini kwa
sasa yamebaki sita tu. Wengi wameamua kuuza kazi za nje mbazo ni nafuu.
Hii ni hatari” alisisitiza Mtitu.
Aliongeza
kwamba pamoja na Serikali kuirasimisha sekta ya filamu bado kuna
changamoto ya kazi zinazotoka nje kutokuwekewa stempu za mamlaka ya
mapato huku kukiwa na uharamia unaotishia bei za filamu halali zenye
stempu hizo.
Jukwaa
la BASATA limekuwa likifanyika kwa mwezi mara mbili siku za Jumatatu na
wiki hii kulikuwa pia na utambulisho wa asasi ya ubalozi wa Utamaduni
wa Mwafrika ambayo imeasisiwa nchini Cameroon, Afrika Magharibi mwaka
2014.
Rais
na mwanzilishi wa asasi ya Mabalozi wa Utamaduni wa Mwafrika (African
Culltural Embassy Association) Bwana Colpas Numfor kutoka nchini
Cameroon (Katikati) akionesha nyaraka mbalimbali za usajili wa asasi
yake wakati akiongea na wadau wa Sanaa kwenye programu ya BASATA ya
Jukwaa la Sanaa. Kushoto kwake ni Katibu wa chama cha waandishi wa
habari za Sanaa na Utamaduni (CAJAtz) Hassan Bumbuli na Kaimu Mkurugenzi
wa asasi hiyo nchini Tanzania Bw. Maganiko Charles.
Msanii na mzalishaji filamu nchini William Mtitu (Kulia) akiongea na wadau wa Sanaa (hawako pichani) wakati akiwasilisha mada iliyohusu ‘Ubora katika filamu na changamoto zake’ kwenye Jukwaa la Sanaa la Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) mapema wiki hii. Kushoto ni Katibu wa chama cha waandishi wa habari za Sanaa na Utamaduni (CAJAtz) Hassan Bumbuli.
"Ask not, what your country can do for you. Ask what, you can do for your country"- JFK.
ReplyDeleteBASATA- nendeni benki, mkaombe mkopo wa miaka 20 au 30, inategemea ni kiasi gani mnahitaji. Mtarudisha mkopo taratibu pamoja na interest, kwani ukumbu ukimalizika utakuwa ni chanzo cha biashara na mapato.
Iacheni Serikali iendelee na mambo meningine kama vile ujenzi wa barabara, madaraja, zahanati, shule NK
Watanzania tuwe wabunifu, tusiwe kama mtoto wa miaka 25 bado anawategemea wazazi wake wampe hela ya kula!
Tuchacharike! tuzisake ngawila.