Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe akitoa hotuba fupi ya uzinduzi wa Magereza "Duty Free Shop" Gereza Kuu Lilungu, Mkoani Mtwara leo Julai 5, 2015 katika Viwanja vya Lilungu, Mkoani Mtwara.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe(kulia) akifurahia jambo wakati wakiwa kwenye jiwe la Msingi mara tu baada ya kuzindua rasmi duka hilo lenye bidhaa zisizo na tozo la Kodi(wa pili kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja(kushoto) ni Mkurugenzi wa Transit Military Shop, Bw. Alfazar Meghji. Uzinduzi huo umefanyika Julai 5, 2015 katika Viwanja vya Gereza Kuu Lilungu, Mkoani Mtwara.
Bidhaa mbalimbali zinazopatikana katika Magereza "Duty Free Shop" ya Gereza Kuu Lilungu, Mkoani Mtwara kama inavyoonekana katika picha. Duka hilo limezinduliwa rasmi na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe(hayupo pichani).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...