Mmoja wa wakina mama kutoka Kikundi cha Wachimbaji Madini Wanawake Tanzania, (Tanzania Women Mining Association) Shamsha Diwani (katikati) akitoa maoni yake mara baada ya kutembelea banda la Kitengo cha Uthamini wa Madini ya Vito na Almasi Nchini ( TANSORT) kwenye maonesho ya kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mtaalam kutoka Kitengo cha Uthamini wa Madini ya Vito na Almasi Nchini ( TANSORT) Dorcus Moshi (katikati) akiwaelimisha watoto waliotembelea banda hilo aina za madini yanayopatikana nchini Tanzania.
Baadhi ya wananchi wakiangalia aina za madini ya mawe katika banda la Wakala wa Jiolojia Nchini (GST), kwenye maonesho ya kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Banda la Wizara ya Nishati na Madini kama linavyoonekana pichani kwenye maonesho ya kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...