KISAKALE CHA BIBI NYAMIHEMBE WA WAZARAMO NI CHIMBUKO LA UTANI WA WAZARAMO NA WANYAMWEZI.

Benjamin Sawe-WHVUM
HADITHI moja ya ajabu inayosimuliwa na wazee wa kizaramo ni ile ya Nyamihembe aliyolewa Unyamwezi,msimulizi mmoja alisema haikuwa Hadithi ya kweli, nayo ni hii, ( Hii ni Tanzu ya Fasihi simulizi)

Mzee mmoja wa Kizaramo alikuwa na binti mzuri aliyeitwa Nyamihembe, mtoto wa kiti cha kwanza,(Mtoto wa kiti ni mwana Nyang’iti, ni utambulisho wa Mila na Desturi za baadhi ya Makabila ya Pwani, hutumika katika shuhuri zote za kimila za kurithisha vijana katika kundi la utu uzima) Baada ya kuvunja ungo akatokea Mnyamwezi mmoja akamposa, na kufunga pamvu(Harusi), kisha akapewa Bibi huyo akaishi naye. 

Lakini Yule Mnyamwezi baadae alipendelea kurudi kwao unyamwezi pamoja na mke yule, basi akataka idhini kwa wazazi akakubaliwa,akaondoka Uzaramo na mkewe hadi kwao Unyamwezini.

Walipokuwa kule wakajaaliwa watoto wengi wa kiume na wakike, waliishi kule Unyamwezi kwa miaka mingi hadi wale watoto wakawa watu wazima, wakaoa na kuolewa, wakazaa watoto kadha wa kadha waliokua wajukuu wa Nyamihembe.

Lakini watoto na wajukuu wa
 Nyamihembe hawakupata bahati ya kufika Uzaramo tangu kuzaliwa kwao ila kila mara bibi Nyamihembe alikuwa akiwasimulia habari za Uzaramo kama hadithi tu.

Nyamihembe aliishi kule hata akawa mzee (ajuza), maana hata wale wajukuu walizaa kisha wakajukuu, akawa na virembwe kadha wa kadha,wakati ule yule Mzazi mwezake Mnyamwezi Uzee ulimkithiri akafariki Dunia. 

Fanani wa Hadithi ni Mwaruka Ramadhani (1965) 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...