Mfanyakazi wa Vodacom Tanzania Jessam Jeremia akiwapa maelekezo baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliofika kwenye gurio la “Vodacom expo” lilioandaliwa na kampuni hiyo kwa ajili ya kuwauzia bidhaa mbalimbali za mawasiliano kwa bei nafuu.Gurio hilo linafanyika kwa siku mbili mfululizo katika viwanja vya Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es Salaam waliofika kwenye viwanja vya Kijitonyama kwenye gurio la Vodacom Expo wakionyeshwa baadhi ya simu na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania ambazo zinauzwa kwa bei nafuu zaidi, Gurio hilo limeandaliwa na Vodacom Tanzania kwa siku mbili mfululizo kwa ajili ya kuwauzia wakazi wa jiji bidhaa za mawasiliano kwa gharama nafuu.
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es Salaam wakinunua bidhaa mbalimbali za mawasiliano kwa bei nafuu kwenye viwanja vya Posta Kijitonyama wakati wa Gurio la Vodacom Expo linalofanyika kwa siku mbili mfululizo.
Meneja bidhaa wa Vodacom Tanzania, Liginiku Milinga akifanyiwa mahojiano na baadhi ya waandishi wa habari waliofika katika Gulio(Vodacom Expo)lililoandaliwa na kampuni hiyo kwa ajili ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam kununua bidhaa mbalimbali za mawasiliano kwa bei nafuu na kufanyika kwa siku mbili mfululizo katika viwanja vya Posta kijitonyama jijini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...