Baadhi ya Mabalozi wa Vodacom Tanzania wanaoenda kutoa elimu kwa wateja wa kampuni hiyo na wananchi kwa ujumla kuhusiana na huduma ya M-Pawa wakimsikiliza Mkuu wa Mawasiliano na Masoko wa kampuni hiyo,Kelvin Twissa wakati wa uzinduzi wa kampeni ya ‘M-Pawa Tumekufikia’ yenye lengo la kuwaelimisha wateja wake nchi nzima kuhusiana na manufaa ya huduma ya M Pawa inayowawezesha kujiwekea akiba na kujipatia mikopo nafuu kwa urahisi zaidi.Uzinduzi huo ulifanyika makao makuu ya kampuni hiyo Mlimani City jijini Dar e Salaam leo.
Mkuu wa Mawasiliano na Masoko wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa(wakwanza kushoto)na Ofisa Mkuu wa Idara ya M-Pesa,Jacques Voogt wakizindua kampeni ya ‘M-Pawa Tumekufikia’ yenye lengo la kuwaelimisha wateja wake nchi nzima kuhusiana na manufaa ya huduma ya M Pawa inayowawezesha kujiwekea akiba na kujipatia mikopo nafuu kwa urahisi zaidi.Uzinduzi huo ulifanyika makao makuu ya kampuni hiyo Mlimani City jijini Dar e Salaam leo.

Wateja wa Vodacom Tanzania na wananchi kwa ujumla wanaonufaika na huduma ya M-Pawa inayotolewa na kampuni hiyo kwa kushirikiana na benki ya CBA itawafikia watanzania wengi zaidi baada ya kampuni hiyo kuzindua kampeni ya kabambe ya ‘M-Pawa Tumekufikia’ yenye lengo la kuwaelimisha wateja wake kuhusiana na faida na jinsi ya kunufaika na huduma hii inayowawezesha kujiwekea akiba na kujipatia mikopo nafuu kwa urahisi zaidi.

Kampeni ya M-Pawa tumekufikia ambayo imezinduliwa leo jijini Dar es Saaam itafanyika nchini nzima ambapo wataalamu wa huduma watapita kila mkoa kutoa elimu juu ya matumizi na manufaa yake kwa ajili ya kujikwamua kimaisha. Wanachi wanaoishi mijini na vijijini watapata fursa ya kuelimishwa kuhusu M-Pawa na huduma nyingine za Vodacom Tanzania. Mbali na elimu, wateja watajipatia zawadi mbalimbali na kupata burudani kabambe kutoka kwa wasanii nguli wa hapa nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...