Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi,Dkt John Pombe Magufuli akihutubia maelfu ya wananchi katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya jioni ya leo,kwenye mkutano wa kampeni ya kuwaomba ridhaa Watanzania ya kuwaongoza katika awamu ya tano.
Dkt Magufuli amesema kuwa serikali atakayoingoza atakapopata
ridhaa ya kuingia Ikulu,itazifanya huduma za Afya kuwa bora na kuwabana
wahudumu wa afya wenye tabia ya kuchukua dawa na kuziuza kwa watu binafsi.
Magufuli ambaye
yupo katika mikoa ya Nyanda za juu kusini katika kampeni ya kusaka nafasi ya
kuwa raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,amesema suala la afya litakuwa
moja ya ajenda zake muhimu atakapoingia madarakani.
Katika hatua nyingine Dkt Magufuli amewaleza wananchi kuwa iwapo watampa ridhaa ya kuiongoza Tanzania,atahakikisha anaanzisha mahakama maalumu ya Mafisadi na Wala rushwa.
Mbunge wa zamani wa jimbo la Kyela Mzee John Mwakipesile akimpigia debe Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli wakati mgombea huyo alipofika jimboni humo kuomba kura za wananchi ili wamchague kuwa rais.Mzee Mwakipesile amesema kuwa anamuunga mkono Dkt Magufuli na atahakikisha anashiriki kikamilifu kuhakikisha mgombea huyo anaibuka na ushindi kwa kishindo.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kyela Dkt Harrison Mwakyembe akimpigia debe Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya jionu ya leo.
Naibu Waziri wa Fedha Mh Mwigulu Nchemba akihutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya,ambapo Mwigulu aliwaomba wananchi hao waliojitokeza kwa wingi kumpigia kura za ndio Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli na hatimae aweze kuiongoza Tanzania katika awamu ya tano kwa sababu ana sifa zoto za kuongoza nchi.
Maelfu ya Wananchi waliojitokeza kwa wingi katika viwanja vya Nzovwe Mbeya jioni ya leo,ambapo Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli aliwahutubia wananchi hao.
Naibu Waziri wa Fedha Mh Mwigulu Nchemba akihutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya,ambapo Mwigulu aliwaomba wananchi hao waliojitokeza kwa wingi kumpigia kura za ndio Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli na hatimae aweze kuiongoza Tanzania katika awamu ya tano kwa sababu ana sifa zoto za kuongoza nchi.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi,Dkt John Pombe Magufuli akihutubia maelfu ya wananchi katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya jioni ya leo,kwenye mkutano wa kampeni ya kuwaomba ridhaa Watanzania ya kuwaongoza katika awamu ya tano,Magufuli amewaambia wananchi hao kuwa atahakikisha huduma za afya zinaimarishwa ipasavyo,katika suala la Elimu Magufu aliwaeleza Wananchi kuwa iwapo watamchagua katika nafasi hiyo ya Urais atahakikisha elimu kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne itatolewa bure,aidha pia amewataka Watanzania kuwa wamoja katika kuhakikisha wanailinda na kuitunza amani iliyopo nchini.
Wananchi wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia katika mkutano wa kampeni katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya.
Wafuasi na wapenzi wa chma cha CCM wakishangilia
Maelfu ya Wananchi waliokusanyika katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika jioni ya leo.
Jicho la samaki katika ubora wake kwenye mkutano wa kampeni za CCM katika viwanja vya Nzonvwe mjini Mbeya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...