Baadhi ya waandishi wa Habari wakiwa katika Mkutano huo.

Umoja wa Mashirika Matano yanaounda ushirika wa Fahamu,Ongea Sikilizwa(FOS) ambayo ni Oxfam,BBC Media Auction, Legal and Human Rights Centre, Restless Development, and VSO leo wamekutana na waandishi wa Habari kwa ajili ya kuzungumzia mambo Mbalimbali yanayohusiana na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2015 na kueleza malengo ya muungano huo.

Akizungumza Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Bi. Jane Foster ambao ndio waandaaji wa Mkutano huo na waandishi wa Habari alisema kuwa Lengo kubwa la Umoja huo ni kusisitiza na kuwaelimisha wananchi wote kwa ujumlan juu ya Uchaguzi mkuu 2015 ambapo Oxfam wao jukumu lao kubwa ni kuwahimiza wanawake na wasichana wadogo  kuelekea uchaguzi Mkuu kama wapiga kura, na ili kuyafikia makundi yote haya waliandaa na wanaendesha Midaharo mbalimbali, kuunda makundi ya wanawake na zaidi wanatumia mitandao ya kijamii kama Facebook na Twitter kuwapa taarifa juu ya uchaguzi.

BBC kwa upande wao wanajukumu la kusimamia mashirika mbalimbali ya utangazaji Nchini Tanzania ikiwa ni pamoja na kuwapa elimu na kanuni za uandishi bora wa Habari za uchaguzi Mkuu 2015 

Nao kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ambao walikuwa na jukumu la Kusimamia zoezi zima la uasdikishaji wa wapiga Kura ambapo walikuwa na watu 165 nchi nzima wakiangalia na kuangalia makosa yaliyojiokeza na kupeleka Maoni yao sehemu husika, na pia katika kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2015 wameandaa kitengo maalumu cha Teknolojia ambacho kitasimamia uchaguzi wote.

BOFYA HAPA KWA PICHA NA HABARI ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...