Mkurugenzi wa Msama Promotions akizungumza na Waandishi wa habari kwenye ofisi za kampuni hiyo,jijini Dar kuhusiana na kuandaa tamasha la kuiombea Tanzania inayoelekea kwenye uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika,Oktoba 25 mwaka huu,Tamasha hilo linatarajia kufanyika Oktoba 4.
KAMPUNI ya Msama Promotions imeandaa Tamasha kubwa la kihistoria ambalo halijawahi kufanyika nchini la kuiombea Tanzania inayoelekea katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25.
KAMPUNI ya Msama Promotions imeandaa Tamasha kubwa la kihistoria ambalo halijawahi kufanyika nchini la kuiombea Tanzania inayoelekea katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25.
Kwa mujibu wa
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions Alex Msama Tamasha hilo
litafanyika Oktoba 4, jijini Dar es
Salaam.
Msama alisema kutokana
na uzito na heshima ya tamasha hilo,
linatarajia kushirikisha waimbaji mbalimbali wa nyimbo za injili wa ndani na
nje ya nchi ambao wanaotamba katika tasnia ya muziki huo.
Alisema japo ni
mara ya kwanza kwa kampuni yake kuandaa tamasha kama hilo katika historia ya uchaguzi nchini,
anaamini kwa vile amani ni kitu muhimu katika uchaguzi, wengi watamuunga
mkono.
Msama alisema
anaamini wengi watajitokeza kuungana pamoja na viongozi wa kitaifa na kada
mbalimbali kuuombea uchaguzi huo ambao ni njia ya kidemokrasia ya kupata
viongozi kwa ngazi ya urais, ubunge na udiwani.
“Watanzania
wajiandae kuiombea amani Tanzania
kupitia muziki wa Injili hasa waimbaji mbalimbali wa kutoka nje ya Tanzania watashiriki katika tukio hilo ambalo bado tuko
katika mchakato wa mahali tutakapofanyia,” alisema Msama na kuongeza:
“Tamasha hilo kubwa kimaudhui
linakaribia Tamasha kubwa la Pasaka ambalo hufanyika kila mwaka tangu mwaka
2000,” alisema Msama aliyechangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa muziki wa injili.
Aidha Msama
alisema baada ya tamasha hilo kufanyika jijini
Dar es Salaam, watahamishia maombi hayo katika majiji mengine manne kwa lengo hilo la kuombea amani na
utulivu uchaguzi Mkuu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...