Mkurugenzi wa Msama Promotions akizungumza na Waandishi wa habari kwenye ofisi za kampuni hiyo,jijini Dar kuhusiana na kuandaa tamasha la kuiombea Tanzania inayoelekea kwenye uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika,Oktoba 25 mwaka huu,Tamasha hilo linatarajia kufanyika Oktoba 4.

KAMPUNI ya Msama Promotions imeandaa Tamasha kubwa la kihistoria ambalo halijawahi kufanyika nchini la kuiombea Tanzania inayoelekea katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions Alex Msama Tamasha hilo litafanyika Oktoba 4, jijini Dar es Salaam.

Msama alisema kutokana na uzito na heshima ya tamasha hilo, linatarajia kushirikisha waimbaji mbalimbali wa nyimbo za injili wa ndani na nje ya nchi ambao wanaotamba katika tasnia ya muziki huo.

Alisema japo ni mara ya kwanza kwa kampuni yake kuandaa tamasha kama hilo katika historia ya uchaguzi nchini, anaamini kwa vile amani ni kitu muhimu katika uchaguzi, wengi watamuunga mkono.
Msama alisema anaamini wengi watajitokeza kuungana pamoja na viongozi wa kitaifa na kada mbalimbali kuuombea uchaguzi huo ambao ni njia ya kidemokrasia ya kupata viongozi kwa ngazi ya urais, ubunge na udiwani.

“Watanzania wajiandae kuiombea amani Tanzania kupitia muziki wa Injili hasa waimbaji mbalimbali wa kutoka nje ya Tanzania watashiriki katika tukio hilo ambalo bado tuko katika mchakato wa mahali tutakapofanyia,” alisema Msama na kuongeza:

“Tamasha hilo kubwa kimaudhui linakaribia Tamasha kubwa la Pasaka ambalo hufanyika kila mwaka tangu mwaka 2000,” alisema Msama aliyechangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa muziki wa injili.

Aidha Msama alisema baada ya tamasha hilo kufanyika jijini Dar es Salaam, watahamishia maombi hayo katika majiji mengine manne kwa lengo hilo la kuombea amani na utulivu uchaguzi Mkuu.   

Alitaja nchi watakazotoka waimbaji watakaosindikiza maombi hayo niAfrika Kusini, Rwanda, Kenya, Uganda, Zambia, Burundi na DR Congo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...