Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mwenyekiti wa Baraza la Usalama Barabarani,
Pereira Ame Silima akizungumza na Wadau wa Usalama Barabarani pamoja na Wajumbe wa
Baraza la Taifa la Usalama Barabarani kutoka mikoa yote nchini katika mkutano wa baraza hilo
ambao unajadili masuala mbalimbali ya jinsi ya kupunguza ajali za barabarani nchini. Kulia ni
Katibu wa Baraza la Usalama Barabarani ambaye pia ni Kamanda wa Kikosi cha Polisi Usalama
Barabarani nchini, Naibu Kamishna wa Polisi, Mohamed Mpinga. Katikati ni Kamishna
Msaidizi wa Jeshi la Polisi nchini Malawi ambaye pia ni Kiongozi wa Kikosi cha Usalama
Barabarani nchini humo, Maepheson Matowe. Mkutano huo ambao unaenda sambamba na
Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani unafanyika katika Hoteli ya Regal
Naivera jijini Tanga.
Sehemu ya Wadau na Wajumbe wa Baraza la Usalama Barabarani kutoka mikoa yote chini
wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa Baraza hilo, Pereira Ame Silima (hayupo pichani)
katika mkutano wa baraza hilo ambao unajadili masuala mbalimbali ya jinsi ya kupunguza ajali
za barabarani nchini. Mkutano huo unaenda sambamba na Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa
Usalama Barabarani unafanyika katika Hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga.
Mtoa mada wa Mkutano Mkuu wa Wadau wa Usalama Barabarani ambaye ni Mkemia Mkuu wa
Serikali, Prof. Samweli Manyele akizungumza na Wadau wa Usalama Barabarani pamoja na
Wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani kutoka mikoa yote nchini katika mkutano
wa baraza hilo ambao unajadili masuala mbalimbali ya jinsi ya kupunguza ajali za barabarani
nchini. Prof. Manyele alitoa elimu ya jinsi ya kusafirisha salama kemikali. Mkutano huo ambao
unaenda sambamba na Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani unafanyika
katika Hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mwenyekiti wa Baraza la Usalama Barabarani,
Pereira Ame Silima (katikati meza kuu) akijadili jambo na Kamanda wa Kikosi cha Polisi
Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna wa Polisi, Mohamed Mpinga, wakati wa Mkutano
Mkuu wa Wadau wa Usalama Barabarani pamoja na Wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama
Barabarani kutoka mikoa yote nchini katika mkutano wa baraza hilo ambao unajadili masuala
mbalimbali ya jinsi ya kupunguza ajali za barabarani nchini. Wengine katika picha ni wajumbe
wa mkutano huo. Mkutano huo ambao unaenda sambamba na Maadhimisho ya Wiki ya Nenda
kwa Usalama Barabarani unafanyika katika Hoteli ya Regal Naivera jijini Tanga. Picha zote
na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...