Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Sherehe ya Siku ya Wahandisi Tanzania mwaka 2015 Prof. Bakari Mwinyiwiwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Wahandisi nchini itakayofanyika Septemba 3 mpaka 4 jijini Dar es salaam.Kulia ni Msajili wa Wahandisi nchini Tanzania Muhandisi Steven Mlote na kushoto ni Msajili msaidizi wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi Tanzania (ERB) Muhandisi Benedict Mukama
Msajili wa Wahandisi nchini Tanzania Muhandisi Steven Mlote (kulia) akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Wahandisi nchini yatakayofanyika Septemba 3 mpaka 4 mwaka huu.
Picha na Aron Msigwa-MAELEZO.
Na.Aron Msigwa - MAELEZO,1/9/2015.Dar es salaam.
KATIBU Kiongozi Balozi Ombeni Sefue anatarajiwa kuwa mgeni rasmi wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Wahandisi nchini Tanzania itakayofanyika Septemba 3 hadi 4 jijini Dar es salaam.
Akizungumza na waandishi wa Habari leo jijini Dar es salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya sherehe hiyo Prof.Bakari Mwinyiwiwa amesema Kuwa Jumuiya ya Wahandisi nchini Tanzania inafanya maadhimisho hayo kwa mara ya 13 toka kuzinduliwa kwake mwaka 2003 kuenzi mchango wa wahandisi katika kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...