

Bw. Husain AlSafi, Mkurugenzi Mkuu wa tawi la Shirika la ndege la Emirates Tanzania ambao walikuwa ni wadhamini wa shindano hilo akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za Skylink.

Msimamizi wa bodi ya Michezo ya kubahatisha nchini, Bw. Abdallah Hemed akizichanganya vipeperushi ili kuwapata washindi wa droo hiyo.

Mwandishi wa habari kutoka TBC akiwa ameshika moja ya kipeperushi cha mteja wa Skylink aliyeibuka mshindi wa kwanza na kujinyakulia gari mpya aina Hyundai ix35 katika droo iliyochezeshwa kwenye ofisi za Skylink Jijini Dar es Salaam.

Ofisa wa Uniglobe Skylink Travel & Tours Bw. Solomon Mwale akiwatangaza washindi waliopatikana kwenye droo iliyofanywa na kampuni ya Skylink leo.

Wafanyakazi wa kampuni ya Uniglobe Skylink Travel & Tours wakiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa kampuni ya Hyundai Tanzania ambao walikuwa ni wadhamini wakuu kwenye shindano hilo
Hassan Taliki mkazi wa Jijini Dar es Salaam leo ameibuka mshindi na kushinda gari mpya aina Hyundai ix35 katika droo iliyochezeshwa kwenye ofisi za Skylink Jijini Dar es Salaam.
Mshindi huyo amepatikana kutokana na kukata tiketi ya ndege katika Kampuni hiyo hivyo ili aweze kupata zawadi hiyo ametakiwa kwenda na kipeperushi Skylink cha tiketi aliyokana na kitambulisho chake kwa maelekezo zaidi.
Washindi wengine walioshinda kwenye droo hiyo ni Mohamed Swala ambaye ameshinda safari ya kwenda Mahinra kwenda na kurudi huku Issa Nassoro ambaye amekuwa mshindi wa tatu amepata tiketi ya kwenda na kurudi Dubai ambako atapelekwa na Kampuni hiyo .
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Ofisa wa Skylink Solomon Mwale alisema kwamba wamepanga kufanya hafla ya kuwakabidhi washindi hao zawadi zao ili umma uweze kuamini kwamba hawabahatishi na droo ikichezeshwa inakuwa ni kweli.
Droo hii ni sehemu ya motisha inayotolewa na Kampuni yetu kwa wateja wote wa Skylink ambao hununua tiketi za usafiri wa ndege kwenda katika nchi mbalimbali duniani.
Droo hiyo imedhaminiwa na Skylink, Hyundai, Emirates, Exim Bank na Club Mahindra.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...