Moja kati ya majengo ya shule ya Msingi Busindi, yaliyomaliziwa kujengwa na mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu ulioko wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga. Mgodi huo unaomilikiwa na kampuni ya Acacia, umekabidhi miradi minne ya elimu na maji yenye thamani ya shilingi bilioni 1 ikiwa ni sera ya kampuni kujenga mahusiano mema na jamii inayozunguka migodi.
Kaimu
Mku wa Wilaya ya Msalala, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kahama mkoani
Shinyanga, Benson Mpesya, Meneja Mkuu Mgodi wa Dhahabu Bulyanhulu, BGML,
Michelle Ash, (katikati) na Mkurugenzi wa Maendeleo Halmashauri ya Wilaya ya
Msalala, wakipapu maji wakati wa uzinduzi rasmi wa kisima kirefu cha maji
kilichojengwa kwa ufadhili wa kampuni hiyo huko Bugarama. BGML, inayomilikiwa
na Kampuni ya Acacia, imekabidhi miradi mine ya elimu na maji kwa Halmashauri
hiyo yote ikiwa na thamani ya shilingi Bilioni 1.
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Msalala, ambaye pia ni
Mkuu wa Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Benson Mpesya, (kushoto),
akiongozana na Meneja Mkuu wa Mgodi wa Bulyanhulu ulioko wilaya ya Msalala
Mkoani Shinyanga, Michelle Ash, (katikati), na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi
Busindi, Joseph Misungwi, baada ya kuzindua moja kati ya nyumba kadhaa za
walimu, zilizojengwa kwa msaada wa mgodi huo. Mhgodi huo unaomilikiwa na
kampuni ya uchimbaji na utafutaji madini, Acacia, umekabidhi halmashauri ya
wilaya hiyo, miradi ya elimu na maji yenye thamani ya shilingi Bilioni 1,
kwenye hafla hiyo iliyofanyika Agosti 31, 2015.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...