Familia ya
Kanali Mstaafu Burchard Mushumbusi, inatoa shukrani za dhati kwa ndugu, jamaa, marafiki na majirani wote
walioshiriki nasi kwa hali na mali katika msiba wa mpendwa wetu Bi. Candida K
Mushumbusi aliyefariki tarehe 24 Julai 2015 katika hospitali ya Apollo, New
Delhi India na kupumzishwa katika nyumba yake ya milele tarehe 28 Julai 2015 hapa
Dar es salaam.
Familia pia
inatoa shukrani za dhati kwa Paroko na Mapadre wa Parokia ya Mt. Nicolaus,
Kunduchi Mtongani; Uongozi na jumuiya ya
Mt. Yohane Mbatizaji Kunduchi; Mkuu wa Majeshi
ya Ulinzi ya Tanzania; Uongozi na watumishi wa Hari Singh&Sons,
Benki Kuu ya Tanzania(BOT), Tanzania Food and Nutrition Centre (TFNC) ,
Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni na
VASTech.
Tunatoa pia
shukrani za pekee kwa Madaktari na wauguzi wote wa hospitali za Apollo New
Delhi; Ruby Hall Clinic na Inamdar za Pune; Shree Hindu Mandal, Lugalo na
Regency Medical Centre;
Hatutaweza
kuwataja wote kwa majina, lakini tunaomba wote mpokee shukrani zetu za dhati
kwa upendo wenu kwa familia hii.
Misa ya
Shukrani itafanyika siku ya Jumapili tarehe 06 Septemba 2015 katika Kanisa Katoliki la Mt. Nicolaus,
Kunduchi Mtongani saa 3:00 asubuhi. Familia inawakaribisha wote siku hiyo
kanisani na baadae saa 6:00 kwenye chakula cha mchana nyumbani kwa Kanali
Mushumbusi, Kunduchi Beach.
Mungu Ailaze
Roho ya Bi. Candida Mahala Pema Peponi.
Apumzike Kwa Amani.
AMINA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...