Na Mwandishi Wetu, Muheza
Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapiduzi (CCM), katika jimbo la Muheza mkoani Tanga, Balozi Adadi Rajabu (Kulia akipokea fomu), amesema atapigana kufa na kupona kuingiza wawekezaji wilayani humo katika nyanja ya kilimo na utalii.

Akizungumza baada ya kunadiwa na mgombea urais wa CCM, John Pombe Magufuli, Adadi amesema mjini hapa jana kwamba ataelekeza nguvu kubwa katika kuvutia wawekezaji ili kuiinua Muheza kiuchumi.

Magufuli, aliyemnadi Adadi kwa kumuita “tunu ya Wanamuheza”, alisema akichaguliwa na kuungwa mkono  Adadi ni mtu mwenye hazina ya  uzoefu adimu na mwenye kuaminiwa na watu na taasisi nyingi ndani na nje ya Tanzania.  Kwa safi hizo ahadi zake ni rahisi kutekelezeka na kuinua   maisha ya wananchi wa Muheza..

Adadi akieleza vipaumbele vyake na mkakati wake wa kuboresha maisha ya watu kiuchumi na kijamii,  aliahidi kupigania kukuza fursa za utalii na kuwepo kwa  viwanda vya kusindika muhogo na matunda, mazao yanayopatikana kwa wingi Muheza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...