Muasisi wa Shirika lisilo la kiserikali
la READ International, Rob Wilson (katikati) akizungumza katikasherehe
za miaka 10 ya shirika hilo jijini Dar es Salaam. Wengine ni baadhi ya
wanachama wa shirika hilo la kujitolea nchini Tanzania. READ
International inatimiza miaka 10 tokea kuanzishwa ikisihirikiana na
Realising Education for Development pamoja na wahisani wengine imeweza
kusaidia ujenzi wa maktaba 72 na kutoa vitabu zaidi ya milioni 1.4
nchini kote.
Mjumbe wa Bodi ya READ International,
Faraja Kotta Nyalandu (kulia), mwanzilishi wa READ, Tom Wilson (wa pili
kushoto) pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Makumbusho
ya jijini Dar es Salaam wakikata keki kusherehekea miaka 10 ya shirika
hilo.
Muasisi wa Shirika lisilo la kiserikali
la READ International, Rob Wilson (kulia) akizungumza na baadhi ya
wanafunzi wa Shule ya Sekondari Makumbusho alipotembelea maktaba ya
shule hiyo iliyowezeshwa kwa ufadhili wa shirika hilo kwa kushirikiana
na Realising Education for Developmentpamoja na wahisani wengine.
READ International inatimiza miaka 10 tokea kuanzishwa huku ikisaidia
ujenzi wa maktaba 72 na kutoa vitabu zaidi ya milioni 1.4 nchini kote.
Wengine pichani ni baadhi ya walimu wa shule hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...