Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid akiangalia kibao cha taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete iliyozinduliwa leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam
 Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid akiogea na mmoja wa wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa moyo katika taasisi hiyo
 Muuguzi akiwa na mmoja wa wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa moyo
 Picha ya pamoja baada ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid  kuizindua  Taasisi hiyo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam  
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid  akizindua Taasisi hiyo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam  
 Taasisi ya Moyo ambayo itajulikana kwa jina la  Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ( The Jakaya  Kikwete Cardiac Institute ) imefunguliwa  rasmi leo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salam.
Taasisi hiyo itatoa mafunzo ya Ubingwa wa juu katika fani ya Upasuaji wa Moyo , dawa ya usingizi na Tiba ya Moyo kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili( MUHAS).
            Akizindua Taasisi hiyo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam kwa niaba ya Rais Jakaya Kikwete, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid  amesema taasisi hiyo  imeleta ahueni  kwa wagonjwa  wa moyo nchini ambapo kati ya Januari hadi Agosti mwaka huu imehudumia wagonjwa wa nje 14, 257 ,wagonjwa waliolazwa ni 912 na imefanya upasuaji kwa wagonjwa 148.
            Kati ya wagonjwa waliofanyiwa upasuaji ,wagonjwa watano tu ndio waliofariki Dunia ambao ni Asilimia 3. 4 , kiwango ambacho ni kidogo kuliko wastani uliokisiwa na wataalam wa asilimia 13.
            Akifafanua amesema huduma zilizotolewa na taasisi hiyo  zimeokoa kiasi cha Shilingi 1, 915,440,000  iwapo wagonjwa hao  wangepelekwa kutibiwa nje ya nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Tuendelee kuimarisha huduma za Afya nchini kote na katika hospitali za rufaa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...