Tunasikitika kuwaarifu kwamba mwenyekiti wetu wa kwanza wa mfuko Mr Michale Mgodo amepatwa na msiba wa baba yake mzazi Marehemu Godfrey Mngodo (pichani) uliotokea katika hospitali ya Dar Group jijini Dar es salaam juzi.
Mipango ya mazishi inafanyika
nyumbani Tanzania na hapa USA kwa Mr and Mrs Mngodo.
Address
yao ni
549 Wildindingo Run,
Westerville,
Ohio 43081.
Kwa maelezo Zaidi please wasiliana na Michael Mngodo kwa kupitia number 614 446 5556, Teddy Mngodo 614 772 1591 na mwenyekiti wa sasa ndugu Deo Mwalujuwa kwa number yake ya 614 378 8655.
549 Wildindingo Run,
Westerville,
Ohio 43081.
Kwa maelezo Zaidi please wasiliana na Michael Mngodo kwa kupitia number 614 446 5556, Teddy Mngodo 614 772 1591 na mwenyekiti wa sasa ndugu Deo Mwalujuwa kwa number yake ya 614 378 8655.
Kama kawaida yetu tunaombwa tufike
nyumbani kwa wafiwa katika kipindi hiki kigumu cha msiba huu.
nyumbani kwa wafiwa katika kipindi hiki kigumu cha msiba huu.
BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA.
Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salamu za rambirambi kuomboleza kifo cha aliyekuwa mmoja wa magwiji wa Tasnia ya Utangazaji nchini Mzee Godfrey Mngodo ambaye alifariki dunia, Ijumaa, Septemba 11, 2015 mjini Dar es Salaam.
Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salamu za rambirambi kuomboleza kifo cha aliyekuwa mmoja wa magwiji wa Tasnia ya Utangazaji nchini Mzee Godfrey Mngodo ambaye alifariki dunia, Ijumaa, Septemba 11, 2015 mjini Dar es Salaam.
Katika
salamu zake za rambirambi kwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,
Dkt. Fenella Mukangara, Rais Kikwete amesema kuwa amesikitishwa na taarifa za kifo
cha Mzee Mngodo ambaye amemweleza kama kielelezo thabiti cha weledi na ubora wa
Tasnia ya Utangazaji katika Tanzania.
“Nimesikitishwa na
kifo cha Mzee Mngodo ambaye kwa kila kigezo alikuwa kielelezo thabiti cha
weledi na ubora wa utangazaji katika nchi yetu. Kwa miaka mingi alichangia sana
maendeleo ya nchi yetu kupitia kazi yake ya utangazaji tokea alipokuwa Redio
Tanzania Dar es salaam (RTD) hadi alipohamia DTV. Tutaendelea kumkumbuka kwa mchango
wake huo kwa taifa letu.”
Rais Kikwete
pia amemtaka Waziri Mukangara kumfikishia pole zake nyingi kwa familia ya Mzee Mngodo
na kuwajulisha kuwa yuko nao katika kumwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema,
aiweke peponi pema roho ya Marehemu Mzee Godfrey Mngodo. Amen.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya
Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...