Mchezaji wa timu ya Ilala Rukia Annaph (kushoto) akichuana vikali na mchezaji wa timu ya Temeke Christina Daudi katika mchezo wa nusu fainali ya Airtel Rising Stars kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam leo (Alhamisi September 17. Temeke ilishinda 2-1
 Mchezaji wa timu ya Ilala Tumaini Michael (Kulia) akimtoka mchezaji wa timu ya Temeke Shamimu Hamis katika mchezo wa nusu fainali ya Airtel Rising Stars kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam leo (Alhamisi September 17). Temeke iliibukana na ushindi wa magoli 2-1.
Mchezaji wa timu ya Ilala Jackline Albert (Kushoto) akimtoka mchezaji wa timu ya Temeke Shamimu Hamis katika mchezo wa nusu fainali ya Airtel Rising Stars kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam leo (Alhamisi September 17. Temeke ilishinda 2-1.

TEMEKE girls jana walifanikiwa kutinga hatua ya fainali, baada ya kuwagaragaza majirani zao wa Ilala kwa kuwafunga mabao 2-1 katika muendelezo wa michuano ya U-17 ya Airtel Rising Stars, mchezo uliofanyika katika uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam.

Ilala ambao walionekana kuumiliki mpira kwa kiasi kikubwa sana katika kipindi cha kwanza walifanikiwa kuandika bao lao mnamo dakika ya 1 baada ya Tumaini Michael kuachia shuti na kutinga wavuni huku kipa wa Temeke akiwa hana la kufanya.

Alamanusra Ilala wapate baola pili manmo dakika ya 20 baada ya Tumaini Michael tena kupiga mpira wa kichwa ambao ulipaa kidogolangoni mwa Temeke.

Katika kipindi cha pili, Temeke walionekana kucharuka huku wakicheza kwa kasi kubwa, na ndipo mshambuliaji wa timu hiyo, Shamimu Hamisi mnamo dakika ya 40, alipomalizia kwa umaridadi mpira uliotemwa na kipa wa Ilala na kuukwamisha moja kwa moja wavuni na kusawazisha goli.
Temeke waliofanikiwa kuandika goli la pili mnamo dakika ya 61 kupitia kwa Asia Juma na kudidimiza matumaini ya Ilala kutinga hatua ya fainali. 

Baada ya mchezo huo kocha wa Ilala Omari Bwezi alisema: “Tumekubali matokeo,wachezajiwangu walicheza vizuri kipindi cha kwanza lakini walionekana luchoka sana kipindi cha pili na kuwapa nafasi ya kutawala wnzetu na ndio maana tukafungwa”.

Naye kocha wa Temeke Daudi Siang’a alisema:  “Vijana wangu walifuata niliyowalekeza wakati wa mapumziko na waliporudi uwanjani walifanya nilichowaeleza na hatimaye tukapata matokeo”.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...