KAMPUNI
YA RELI TANZANIA
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI YA KUAHIRISHA SAFARI YA TRENI
KWENDA BARA LEO IJUMAA SEPTEMBA 11, 2015, HADI KESHO
JUMAMOSI SEPTEMBA 12, 2015 SAA 11 JIONI!
Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL unasikitika kuwataarifu
abiria wote na wananchi kwa jumla kuwa kutokana na ajali ya treni ya mizigo
iliyotokea kati ya Ngerengere na Kinonko jana mkoa wa Morogoro , safari ya treni ya abiria kwenda Bara iliopangwa kuondoka leo saa 11 jioni imeahirishwa hadi kesho
Jumamosi Septemba 12, 2015 saa 11 jioni.
Mafundi wa TRL wako katika eneo la ajali tokea jana wakifanya kazi kwa lengo
la kuhakikisha njia inafunguliwa kwa
wakati ili huduma ya treni za kampuni
zirejeea kama kawaida mapema hapo kesho.
Uongozi wa TRL unawaomba radhi wale wote watakaopatwa na
usumbufu wowote utakaojitokeza.
Atakaye soma taarifa
hii amwarifu na mwenziwe!
Imetolewa
na Ofisi ya Uhusiano kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Mhandisi Elias
Mshana
TRL Makao
Makuu,
Dar es
Salaam.
Septemba
11, 2015
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...