Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga (katikati) akimsikiliza Afisa Balozi wa China anayehusika na masuala ya Utamaduni nchini Tanzania Bw. GAO WEI (wapili kushoto) walipofika katika ofisi za Wizara kutambulisha uongozi mpya na kutoa nafasi kwa uongozi wa zamani kuaga Wizara yenye dhamana na masuala ya Utamaduni leo Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga (kulia) akimkabidhi Afisa Balozi wa China aliyemaliza muda wake katika masuala ya Utamaduni nchini Tanzania Bw. LIU DONG zawadi ya picha ya Tingatinga kama ishara ya kumpongeza kwa kuhamasisha mahusiano mazuri ya kiutamaduni kati ya Tanzania na China leo Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga (kulia) akiangalia vitu mbalimbali vya
kiutamaduni alivyokabidhiwa na Afisa Balozi wa China aliyemaliza muda wake
katika masuala ya Utamaduni nchini Tanzania Bw. LIU DONG (katikati) leo Jijini
Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Balozi wa China anayehusika na masuala ya
Utamaduni nchini Tanzania Bw. GAO WEI
Picha na:
Genofeva Matemu - Maelezo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...