Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mama Sihaba Nkinga akizungumza wakati wa uzinduzi wa Tanzania Media Foundation - Mfuko wa Habari Tanzania - TMF) uliyofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa LAPF Millennium Tower jijini Dar es Salaam. Mfuko huu unachukua nafasi ya Tanzania Media Fund
Mwenyekiti wa Bodi ya TMF Mama Halima Shariff akitoa neno la shukurani baada ya bodi hiyo kuzinduliwa usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa LAPF Millennium Tower jijini Dar es Salaam. .
Mkurugenzi wa TMF Bw. Ernest Sungura akizungumza na wadau mbalimbali waliohudhuria katika Uzinduzi wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF) uliyofanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa LAPF Millennium Tower jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa TMF Bw. Ernest Sungura akimpongeza Mkurugenzi wa Shirika la habari la Daraja Bw. Simon Mkina wakati wakati uzinduzi huo wa Mfuko wa Habari Tanzania
Mrisho Mpoto akitumbwiza wakati wa uzinduzi wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF) iliyofanyika leo katika ukumbi wa Millenium Tower jijjini Dar Es Salaam.
Wajumbe wapya wa Bodi ya TMF katika picha ya pamoja wakati wa uzinduzi huo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Mama Sihaba Nkinga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wapya wa Bodi ya TMF na watendaji wa mfuko huo usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa LAPF Millennium Tower jijini Dar es Salaam.
Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii
You have a Solid Board! Most People I know, are results oriented and with integrity.
ReplyDelete