Wanawake wameaswa kukipenda chama cha mapinduzi kwakuwa ndicho chama pekee kitakachowaletea maendeleo yanayotakiwa kwakuwa kinajua changamoto zinazo wakabili wananchi katika kipindi hiki. 

  
Akizungunguza na  wanawake wa wa Kata ya Makolongoni Mbunge wa viti maalum mkoani Iringa Rose Tweve  aliwataka wananchi kutobabaishwa na wapinzani kwani hawana nia njema na watanzania  na kusema kuwa chama hicho kina misingi ya kutetea amani ya Nchi.
 
"sisi sote ni wanawake niwaombeni sana tukipigie kura chama cha mapinduzi kiweze kupata ushindi wa kishindo leo katika chama kuna mgombea mwenza mwanamke tazama hamsini kwa hamsini wahamasisheni vijana wenu pia waelezeni mazuri yalimo ndani ya ccm bila kuwaambia wataendelea kurub uniwa na kutumiwa kwa faida za wachache" alisema rose
  

Alisema huu ndiyo wakati wa wanawake kujitokeza kwa wingi kukiunga mkono chama cha mapinduzi kwa kuwapigia kura wagombea wanaotokana na chama hicho kwakuwa kukipa nchi chama cha Upinzani ni kujisaliti wenyewe hiyo aliwaomba wanawake kuhakikisha wanakisaidia chama cha mapinduzi kiweze kushinda.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...