Afisa Elimu kutoka  Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya Moza Makumbuli akuzungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu  ya  chanzo kikubwa cha uvunjifu wa amani  nchini unatokana na vijana wanaotumia dawa za kulevya, katika Kongamano la vijana wa kitanzania  kweye ukumbi wa Karemjee  jijini Dar es Salaam. 
Baadhi ya vijana walio shikiriki katika mkutano huo kweye ukumbi wa Karemjee jijini Dar es Salaam
 Picha na Emmanuel  Massaka wa Global ya jamii

IMEELEZWA kuwa chanzo kikubwa cha uvunjifu wa amani  nchini unatokana na vijana wanaotumia dawa za kulevya.

Hayo yamelezwa  Jijini dar es Salaam na Mwenyekiti wa Taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Care & Help Bi Karyn David wakati wa Kongamano mahususi lilojadili changamoto za kijamii na uchumi zinazowakabili vijana wa kitanzania hasa wa kike.

Aidha Bi. Karyn amesema kwa sasa jamii imekuwa ikikumbana na tatizo la uvunjfu wa amani kutokana na vijana kujihusisha na utumiaji wa dawa za kulevya.

Amendelea kufafanua kuwa Madhara ya dawa za kulevya ni makubwa kwani yanachangia kuleta utegemezi kwa kuwafanya vijana kushindwa kufanya kazi za kuwaletea maendeleo.

Amebainisha kuwa taarifa za Tume ya Udhibiti wa Dawa za kulevya,kwa manispaa yaKindoni,kwa mwaka 2014 imeonyeshwa kwamba kati ya watumiaji wa dawa za kulevya wa jinsi ya kike asilimia 75 kati yao wengi wakiwa na maambukizi  ya virusi vya Ukimwi.

Amesema kwamba maisha ya kijana wa kike wa Kitanzania huanza kupoteza Mwelekeo tokea siku za utotoni za kijana husika, Kwa upande wake  Mratibu  wa uaswa wa Jinsia katika mwitikio wa udhibi wa virus vya Ukimwi toka Tume ya kupambana na Ukiwi nchini TACAIDS,bwana Jacob Kayomba.
Amesema kwa sasa Jamii inapashwa kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya kwa kudai ndio yamekuwa chanzo kikubwa cha ugonjwa wa ukimwi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...