SenSei Rumadha Fundi, amesimama mbele ya bendera ya Tanzania.
Wakicheza Kata ya kundi kwa pamoja "Shisochin Kata"
Wakuu matawi nchi shiriki.
Kundi la wawakilishi sita wa nchi za Ulaya.
Gasshuku au semina ya Karate mtindo wa Okinawa Goju Ryu
Jundokan So Honbu, imefungwa Jumapili usiku na kufuatiwa kwa
tafrija kubwa ya kuwaaga washiriki "Sayonara Party" wa kike
na kiume, umri kuanzia miaka 13 had 70 toka nchi mbalimbali
za Ulaya na Japan ikiwemo na Tanzania iliyowakilishwa na
sensei Rumadha. Viongozi wa Karate wa nchi zilizoshiriki ni:
sensei Rene Ramanitrandrasana 9 Dan wa Ufaransa,
Sensei Antoine, Ufaransa 5 Dan, Sensei Bob Honiball 8 Dan
Uingereza, Sensei Tony Green 8 Dan , Uingereza, Sensei
Jenni 5 Dan, Uingereza, Sensei Ilpo, Sweden, 7 Dan,
Sensei Caideiro 5 Dan, Ureno, Sensei Dr. Freidrich Gsodam 9
Dan, Austria.
Hii ilikuwa ni semina kubwa ya kipekee kufanyika
Uingereza na wakuu wake wa tano kushiriki toka visiwa vya
Okinawa; walio ongozwa na mwenyekiti wa sasa wa mtindo huo
Sensei Yoshihiro Miyazato, Kancho.
Mbinu na matumizi yake ya kujihami kutumia sanaa ya Karate
pamoja na ubora wa kata zilifanyiwa mazoezi sana katika
semina hiyo.
Kuzingatia nidhamu na utamaduni wa jadi wa
Karate na kuheshimu desturi zake halisi, viongelewa
katika mfumo huo wa Goju Ryu Karate.
Kwa ujuml, semina
hiyo iliwakutanisha washiriki wapatao 120,
wakiwemo na watoto wa umri wa kuanzia miaka 13 had 17.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...