MARA  kadhaa  linapoibuka  suala  la  kugawana  mali  pale  ndoa  inapohesabika  kushindikana   masuala  kadhaa  ya  msingi  na  yanayohitaji  uelewa  huwa  yanaibuka. Moja  ya  suala  kati  ya  masuala  ambayo  huibuka  ni  hili  la  kutenganisha  na  kufafanua  hadhi  ya  mali  za  wanandoa  ili  mgawanyo uweze  kufanyika  kwa  haki. Yawezekana  mwanandoa  akadhani  ana  haki  katika  mali  fulani  lakini  kumbe  kisheria  hana  haki  hiyo  ni mtazamo  wake  ndio  unamsukuma  kuamini  hivyo. 

Halikadhalika  yawezekana  mwanandoa  kudhani  hana  haki  katika  mali  fulani  kumbe  anayo  haki.  Ili kujua    una  haki  ipi katika  mali  ipi  na  huna  haki  katika  mali  ipi yahitajika  kujua  misingi  ya kisheria  inayotumika  kugawanya   mali  za  wanandoa.

1.KUGAWANA  MALI  ZA  WANANDOA.
Ieleweke  kuwa  tunapoongelea  wanandoa  kugawana  mali  tunaongelea  talaka. Hakuna  kugawana  mali  bila  talaka. Na  kisheria  talaka  inapotoka  tu swali linalofuata ni  habari  ya  mali  na  watoto  kama  wapo.  Mali  si  lazima  magari  na  manyumba  lakini  pia hata  vyombo  vya  ndani  vikiwemo  vitanda, makabati, sahani  n,k  nazo  ni  mali  kwa  mujibu  wa  sheria. Navyo  huhitaji mgao.

2.  JE  KUGAWANA  MALI  NI  NUSU  KWA NUSU ?.
Linapokuja  suala  la  kugawana  mali  wengi hudhani mtindo unaotumika  kugawa  ni  ule  wa    nusu  kwa  nusu.  Jambo  hili  si  kweli  kwakuwa  sheria  ya  ndoa 1971 iliyofanyiwa  marekebisho  2002  haisemi  kuwa  utaratibu  wa  kugawana  mali  ni nusu  kwa  nusu. Sheria  hii  imeweka  msingi  mkuu  wa  kugawana  mali  ambao  ndio  hutumika  katika  mahakama  zetu  katika  kutoa  maagizo  ya  kugawa  mali  za  wanandoa.  
Kusoma Zaidi soma bofya HAPA  AU BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...