Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli
akiwaambia wananchi wa Karatu katika mkutano wa kampeni uliofanyika
katika uwanja wa Bwawani,kuwa mmoja wa viongozi wa upinzani anayempenda
kwa dhati, ni aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dkt Wilbrod Slaa,amesema kuwa ni kiongozi imara asiyependa kuyumbshwa na kwamba ni kiongozi anayeweza kuwa na msimamo thabiti na mapenzi makubwa na nchi yake Tanzania.
Umati
wa Washabiki na wafuasi wa CCM waliokusanyika katika uwanja wa Bwawani
jioni ya leo kwenye mkutano wa kampeni mjini
Karatu,wakishangilia mara baada kumsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli alipokuwa akimwaga sera zake huku akijinadi
na kuomba ridhaa ya kuiongoza nchi katika kipindi cha awamu ya tano kwa
nafasi ya Urais.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwanadi wagombea Viti vya Udiwani mbele ya
umati wa wakazi wa mji wa Karatu jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara
wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Bwawani mjini humo mkoani
Arusha.
Mgombea
Uubunge jimbo la Karatu Dk.Wilbald Slaa Lorri akimuombea kura Mgombea
Urais wa CCM Dkt Magufuli pamoja na yeye mbele ya wakazi wa mji wa
Karatu jioni ya leo kwenye mkutano wa kampeni,kulia kwake ni Wabunge
watarajiwa viti maalum wanaowakilisha wanawake mkoa wa Arusha, kushoto ni Catherine Magige na Violet Mfuko wakishangilia.
Mgombea
urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli pichani kushoto
akiungana na wasanii Chege na Temba kucheza muziki wakati wa mkutano wa
kampeni mjini Karatu, mkoani Arusha.
Mgombea
urais wa Tganzania kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia
wananchi katika mkutano wa kampeni mjini Mbulu, mkoani Manyara jioni ya
leo
Dkt. Magufuli akisisitiza jambo mbele ya maelfu ya wananchi wa Mbulu jijini jioni ya leo kwenye mkutano wa kampeni.
Mgombea
Urais wa CCM Dkt Magufuli akiwanadi wagombea ubunge na madiwani mbele
ya wakazi wa mji wa Mbulu kwenye mkutano wa kampeni jioni ya leo.
CCM Songambele tunakutakia ushindi.
ReplyDelete