Kaimu katibu mtendaji wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) Dkt.Adolf Rutayuga akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari hawapo (pichani) wakati alipokuwa akiongea nao makao makuu ya ofisi hizo yaliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam, kuhusiana na maamuzi mbalimbali yaliyofanywa na baraza hilo katika kuratibu uendeshaji wa mafunzo ya elimu ya ufundi nchini. Kushoto ni Mkurugenzi wa Ukaguzi na ufuatiliaji wa Ubora wa Mafunzo wa (NACTE) Agnes Ponera na Msaidizi wa Katibu Mtendaji wa Baraza hilo ,Alex Nkondola.
Waandishi wa habari wakimsikiliza Kaimu Katibu mtendaji wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) Dkt.Adolf Rutayuga wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,juu ya maamuzi mbalimbali yaliyofanywa na baraza hilo katika kuratibu uendeshaji wa mafunzo ya elimu ya ufundi nchini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...